DAVID MOYES ATOA LA MOYONI KUHUSU VAN GAAL NDANI YA MANCHESTER UNITED



DAVID MOYES ATOA LA MOYONI KUHUSU VAN GAAL NDANI YA MANCHESTER UNITED
Hatimaye kocha wa zamani wa Everton na Manchester United, David Moyes ametoa mtazamo wake kuhusu kocha wa sasa wa  United Louis van Gaal.

David Moyes amesema Van Gaal anastahili kupewa muda zaidi huku akiamini kuwa Manchester United inaweza kuzoa mafanikio chini ya Mdachi huyo.

Mashabiki wa United tayari wamepoteza imani kwa Van Gaal huku wakishuhudia klabu yao iliyokosa soka la kuburudisha ikifunga magoli 13 tu msimu huu kwenye Premier League.

Lakini licha ya shutuma za mashabiki na wachambuzi wa soka, Moyes amedai mbadala wake huyo anapitia matatizo yale yale aliyopitia yeye katika uongozi wake wa miezi kumi.

"Baada ya Sir Alex kustaafu, kazi ikawa ni ngumu mno," anaeleza Moyes. "Ilihitaji muda kuijenda upya timu, ilikuwa ni kazi ya kuijenga  Manchester United. Unapaswa pia kukumbuka kuwa David Gill ambaye alikuwa mhimili mkubwa wa timu naye pia aliondoka.

"Nadhani hata utamaduni wa Manchester United uko hivyo, kuwapa muda na kuwasapoti makocha wake. Nina imani watafanya hivyo kwa Van Gaal, anastahili kupewa muda zaidi.

"Bado kuna kazi anayoitengeneza, amefanya usajili ambao nao unahitaji muda kabla haujazaa matunda. Kwa uzoefu nilioupata Hispania inachukua muda wachezaji wa nje kuzoea mazingira mapya."
David Moyes has backed                  under-fire Manchester United manager Louis van Gaal
David Moyes amemtetea kocha wa Manchester United  Louis van Gaal
Van Gaal has not recorded a                  win as United manager since beating Watford at Vicarage                  Road on November 21
Van Gaal hajaipa ushindi United tangu alipoifunga Watford  Novemba 21



Comments