BAYERN MUNICH YAMPA MKONO WA KWA HERI PEP GUARDIOLA, YAMSAINISHA MIAKA MITATU CARLO ANCELOTTI ...Man City sasa ishindwe yenyewe



BAYERN MUNICH YAMPA MKONO WA KWA HERI PEP GUARDIOLA, YAMSAINISHA MIAKA MITATU CARLO ANCELOTTI ...Man City sasa ishindwe yenyewe
Mtendaji mkuu wa Bayern Munich  Karl-Heinz Rummenigge amethibitisha kuwa kocha Pep Guardiola anaondoka mwishoni mwa mismu huu na nafasi yake itazibwa na Carlo Ancelotti.

Habari hizo ni njema kwa Manchester City ambao wanatajwa kuwa mbioni kumnyakua Pep Guardiola mwenye umri wa miaka 44.

Guardiola, ambaye ameshinda taji la Bundesliga mara mbili mfululizo tangu alipotua Allianz Arena, amemua kwenda kusaka changamoto mpya pindi msimu huu utakapokamilika huku klabu yake ikiwa kwenye nafasi nzuri ya kutetea taji lake kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Carlo Ancelotti ambaye amesaini mkataba wa miaka mitatu ya kuikochi Bayern Munich, hakuwa na timu yoyote tangu alipotemwa na Real Madrid wiki chache kabla msimu huu haujaanza.
Pep                  Guardiola sits on the bench during Bayern Munich's match                  away to Hannover 96 on Saturday
Pep Guardiola anaondoka Bayern
Guardiola shows his frustrations on the touchline                  as he watches his Bayern Munich side in action
Guardiola akiwa mzigoni
Carlo                  Ancelotti (pictured hugging Guardiola in 2014) will take                  over the reins at the Bundesliga champions
Carlo Ancelotti (akikumbatiana na Guardiola in 2014) atakuwa kocha wa Bayern msimu ujao
Bayern                  Munich tweeted news of Guardiola's exit in the summer on                  their English Twitter account 
Bayern Munich imetupia habari ya kuthibitisha kuwa Guardiola ataondoka mwishoni mwa msimu huu
Italian manager Ancelotti                  has put pen to paper on a three-year contract at the                  Bundesliga champions 
 Ancelotti amesaini mkataba wa miaka mitatu kuifundisha Bayern Munich
Ancelotti tweeted this picture and message                  following news of his appointment as Bayern manager
Ancelotti ameweka kwenye ukurasa wake wa Twitter picha yake iliyoandamana na maneno yanaoonyesha kuwa ni heshima kubwa kwake kupata nafasi ya kuifunisha Bayern Munich

MATAJI YA GUARDIOLA  NA ANCELOTTI

PEP GUARDIOLA: Barcelona – La Liga: 2008–09, 2009–10, 2010–11, Copa del Rey: 2008–09, 2011–12, Spanish Super Cup: 2009, 2010, 2011, Champions League: 2008–09, 2010–11, Super Cup: 2009, 2011, FIFA Club World Cup: 2009, 2011
Bayern Munich – Bundesliga: 2013–14, 2014–15, German Cup: 2013–14, UEFA Super Cup: 2013, FIFA Club World Cup: 2013
CARLO ANCELOTTI: Juventus (1999–2001) – UEFA Intertoto Cup: 1999
AC Milan (2001–2009) – Champions League: 2002–03, 2006–07, UEFA Super Cup: 2003, 2007, FIFA Club World Cup: 2007, Serie A: 2003–04, Coppa Italia: 2002–03, Italian Super Cup: 2004
Chelsea (2009–2011) – Premier League: 2009–10, FA Cup: 2009–10, Community Shield: 2009
Paris Saint-Germain (2011–2013) – Ligue 1: 2012–13
Real Madrid (2013–2015) – UEFA Champions League: 2013–14, UEFASuper Cup: 2014, FIFA Club World Cup: 2014, Copa del Rey: 2013–14





Comments