Mohamed Elneny anatarajiwa kufanya vipimo vya afya Jumanne hii huko Paris Ufaransa kuelekea usajili wa kujiunga na Arsenal.
Kiungo huyo wa Basle atatua Arsenal kwa dili la pauni milioni 7.4 lakini atapaswa kwanza kusubiri kukamilika kwa hati yake ya kufanya kazi Uingereza kabla usajili huo haujatangazwa rasmi.
Mohamed Elneny mwenye umri wa miaka 23 alirejea Switzerland siku ya mkesha wa Christmas akitokea Misri kwenye mapumziko wakati klabu hizo mbili zikiwa kwenye mazungumzo.
Mchezaji wa kimataifa wa Misri aliyeichezea nchi yake mechi 36, anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne na nusu Arsenal.
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amedhamiria kufanya usajili katika dirisha dogo ili kuziba mapengo ya kikosi chake kilichojaa majeruhi ili kuhakikisha timu yake inakaa kwenye mazingira mazuri ya kupigania taji la Premier League.
Kiungo wa Basle Mohamed Elneny anategemewa kufanya vipimo vya afya Jumanne Arsenal
Mohamed Elneny (kulia) anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne na nusu Arsenal
Comments
Post a Comment