ARSENAL YAKARIBIA KUMNASA MOHAMED ELNENY KWA PAUNI MIL. 7.4 …kufanya vipimo vya afya Jumanne



ARSENAL YAKARIBIA KUMNASA MOHAMED ELNENY KWA PAUNI MIL. 7.4 …kufanya vipimo vya afya Jumanne
Mohamed Elneny anatarajiwa kufanya vipimo vya afya Jumanne hii huko Paris Ufaransa kuelekea usajili wa kujiunga na Arsenal.

Kiungo huyo wa Basle atatua Arsenal kwa dili la pauni milioni 7.4 lakini atapaswa kwanza kusubiri kukamilika kwa hati yake ya kufanya kazi Uingereza kabla usajili huo haujatangazwa rasmi.

Mohamed Elneny mwenye umri wa miaka 23 alirejea Switzerland siku ya mkesha wa Christmas  akitokea Misri kwenye mapumziko wakati klabu hizo mbili zikiwa kwenye mazungumzo.

Mchezaji wa kimataifa wa Misri aliyeichezea nchi yake mechi 36, anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne na nusu Arsenal.

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amedhamiria kufanya usajili katika dirisha dogo ili kuziba mapengo ya kikosi chake kilichojaa majeruhi ili kuhakikisha timu yake inakaa kwenye mazingira mazuri ya kupigania taji la Premier League.
Basle midfielder Mohamed                  Elneny will undergo a medical on Tuesday in Paris ahead                  of joining Arsenal
Kiungo wa Basle  Mohamed Elneny anategemewa kufanya vipimo vya afya Jumanne Arsenal
The 23-year-old (right) is                  expected to sign a four-and-a-half year contract once he                  has obtained a work visa
Mohamed Elneny (kulia) anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne na nusu Arsenal




Comments