Arsenal imedhihirisha kuwa safari              hii haitaki kuwa msindikizaji baada ya kuichapa Manchester              City 2-1 katika mchezo wa Premier League uliochezwa Jumatatu              usiku kwenye uwanja wa Emirates.
        Ikitandaza soka la kutakata,              Arsenal ikafunga magoli yake mawili katika kipindi cha              kwanza kupitia kwa Theo Walcott dakika ya 33 na Olivier              Giroud dakika ya 45.
        Kwa ushindi huo, Arsenal              inayoshika nafasi ya pili kwa kujikusanyia pointi 36,              imepunguza pengo la pointi kati yake na vinara Leicester              City yenye pointi 38.
        Bao pekee la Manchester City              liliwekwa kimiani na kiungo Yaya Toure katika dakika ya 82.
        Mesut Ozil              ndiye aliyetia fora kwa kutengeneza magoli yote mawili ya              Arsenal, hatua inayomfanya awe mpishi wa magoli 14 katika              mechi 10 zilizopita.
        Arsenal (4-2-3-1): Cech;            Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal; Ramsey, Flamini;            Walcott (Chambers 88), Ozil (Oxlade-Chamberlain 76), Campbell            (Gibbs 70); Giroud
        Manchester City (4-3-2-1): Hart;            Sagna, Otamendi, Mangala, Kolarov; Fernandinho, Toure, Delph            (Sterling 46); De Bruyne, Silva (Navas 73); Aguero (Bony 63)
        Theo Walcott akiifungia              Arsena bao la kwanza kufuatia pasi ya kichwa ya Mesut Ozil 
        Walcott akiwapa saluti              mashabiki
        Olivier Giroud anafunga              bao la pili mbele ya beki wa Manchester City  Nicolas              Otamendi 
        Kitendo bila kukosea,              Giroud anamchambua kipa Joe Hart 
        Giroud mwenye umri wa              miaka 29 anashangilia bao lake 
          
Comments
Post a Comment