ARSENAL YA MSIMU HUU WEKA MBALI NA WATOTO, YAIBANJUA MANCHESTER CITY 2-1 ... Mesut Ozil ni balaa



ARSENAL YA MSIMU HUU WEKA MBALI NA WATOTO, YAIBANJUA MANCHESTER CITY 2-1 ... Mesut Ozil ni balaa

Arsenal imedhihirisha kuwa safari hii haitaki kuwa msindikizaji baada ya kuichapa Manchester City 2-1 katika mchezo wa Premier League uliochezwa Jumatatu usiku kwenye uwanja wa Emirates.

Ikitandaza soka la kutakata, Arsenal ikafunga magoli yake mawili katika kipindi cha kwanza kupitia kwa Theo Walcott dakika ya 33 na Olivier Giroud dakika ya 45.

Kwa ushindi huo, Arsenal inayoshika nafasi ya pili kwa kujikusanyia pointi 36, imepunguza pengo la pointi kati yake na vinara Leicester City yenye pointi 38.
Bao pekee la Manchester City liliwekwa kimiani na kiungo Yaya Toure katika dakika ya 82.

Mesut Ozil ndiye aliyetia fora kwa kutengeneza magoli yote mawili ya Arsenal, hatua inayomfanya awe mpishi wa magoli 14 katika mechi 10 zilizopita.

Arsenal (4-2-3-1): Cech; Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal; Ramsey, Flamini; Walcott (Chambers 88), Ozil (Oxlade-Chamberlain 76), Campbell (Gibbs 70); Giroud

Manchester City (4-3-2-1): Hart; Sagna, Otamendi, Mangala, Kolarov; Fernandinho, Toure, Delph (Sterling 46); De Bruyne, Silva (Navas 73); Aguero (Bony 63)

Theo Walcott sumptuously                  whips in the Arsenal opener over the head of Mesut Ozil                  - brilliantly captured by Sportsmail's Andy Hooper
Theo Walcott akiifungia Arsena bao la kwanza kufuatia pasi ya kichwa ya Mesut Ozil 
Walcott salutes the home                  crowd after the 33rd-minute goal against Manchester                  City, with Ozil offering directions to his defenders
Walcott akiwapa saluti mashabiki
Olivier Giroud stole half a                  yard on Manchester City defender Nicolas Otamendi to                  drive home a second on the stroke of half-time
Olivier Giroud anafunga bao la pili mbele ya beki wa Manchester City  Nicolas Otamendi 
Giroud looks on expectantly                  as his powerful shot flies through the legs of a                  helpless Joe Hart in the City goalĀ 
Kitendo bila kukosea, Giroud anamchambua kipa Joe Hart 
The 29-year-old wheels away                  jubilantly with Otamendi crestfallen as Arsenal took                  control of proceedingsĀ 
Giroud mwenye umri wa miaka 29 anashangilia bao lake 








Comments