ARSENAL SASA YAPANIA KUMNASA GANZALO HIGUAIN



ARSENAL SASA YAPANIA KUMNASA GANZALO HIGUAIN
Serie A's leading            scorer Gonzalo Higuain failed to find the net for a ninth            consecutive home match
WASHIKA mitutu wa  London, Arsenal, wameapa kula sahani moja na timu zinazomwania straika wa timu ya Napoli ya Italia, Gonzalo Higuain.

Taarifa za masuala ya usajili ndani ya Arsenal zinasema kuwa, Gonzalo anapewa nafasi kubwa ya kutua Emirates katika usajili wa mwezi Januari, mwakani.

Wenger amebainisha kuwa kipaumbele chake kwa sasa ni kuimarisha kikosi kwa kumpata mlinzi wa kati, mlinda mlango na mshambuliaji.

Gonzalo pia anawaniwa na timu mbalimbali za England, ikiwamo Manchester United na Chelsea, lakini Wenger anatajwa kuwa anaamini  klabu yake itapambana kwa ajili ya kunasa saini ya mshambuliaji huyo.





Comments