WASHIKA mitutu wa  London, Arsenal, wameapa kula sahani            moja na timu zinazomwania straika wa timu ya Napoli ya Italia,            Gonzalo Higuain.
        Taarifa za masuala ya usajili ndani ya Arsenal zinasema            kuwa, Gonzalo anapewa nafasi kubwa ya kutua Emirates katika            usajili wa mwezi Januari, mwakani.
        Wenger amebainisha kuwa kipaumbele chake kwa sasa ni            kuimarisha kikosi kwa kumpata mlinzi wa kati, mlinda mlango na            mshambuliaji.
        Gonzalo pia anawaniwa na timu mbalimbali za England,            ikiwamo Manchester United na Chelsea, lakini Wenger anatajwa            kuwa anaamini  klabu yake itapambana kwa ajili ya kunasa saini            ya mshambuliaji huyo.
        
Comments
Post a Comment