CHELSEA YACHARUKA IKUA 4-0 LIGI YA MABINGWA, PORTO YASHIKWA PABAYA ...kundi lao bado halitabiriki



CHELSEA YACHARUKA IKUA 4-0 LIGI YA MABINGWA, PORTO YASHIKWA PABAYA ...kundi lao bado halitabiriki
Chelsea playmaker            Oscar celebrates with the ball under his shirt as he looks to            the sky in celebration of his 77th minute goal
Mabao yaliyofungwa na Gary Cahill, Willian, Oscar na Kurt Zouma yameipa Chelsea pointi tatu muhimu kufuatia ushindi wake wa 4-0 dhidi ya Maccabi Tel Aviv katika mchezo wa kundi wa Ligi ya Mabingwa.

Wakati Chelsea ikiua 4-0, Porto iliyokuwa inaongoza kundi G, imeshushwa hadi nafasi ya pili baada ya kufungwa 2-0 na Dynamo Kyiv.

Porto na Chelsea zote zina pointi 10, lakini mabingwa hao wa England wanaogoza kundi G kwa wastani mzuri wa magoli.

Dynamo Kyiv ni tatu kwa pointi zake 8 na kufanya nafasi ya kufuzu kwenda 16 bora iwe wazi kwa timu zote tatu za juu kutegemea na matokeo yao ya mwisho yatakavyokuwa Disemba 9 ambapo Chelsea itaumana na Porto na huku Maccabi Tel Aviv wakiwa uso kwa uso na Dynamo Kyiv.

Msimamo wa kundi G huu hapa.



Comments