ZAHA ASEMA ALISOTESHWA BENCHI MANCHESTER UNITED KWA KUPAKAZIWA KUTOKA KIMAPENZI NA BINTI WA DAVID MOYES



ZAHA ASEMA ALISOTESHWA BENCHI MANCHESTER UNITED KWA KUPAKAZIWA KUTOKA KIMAPENZI NA BINTI WA DAVID MOYES
Wilfried Zaha mchezaji wa mwisho kusajiliwa na Sir Alex Ferguson, amesema miongoni mwa sababu ya kupigwa benchi na David Moyes ni shutuma zilizoibuliwa kuwa alitoka kimapenzi na binti wa kocha huyo aitwae Lauren.

Januari mwaka 2013 Ferguson alimsajili Zaha kwa pauni milioni 15 kutoka Crystal Palace lakini akamwacha kwa mkopo Palace hadi mwishoni mwa msimu.

Mrithi wa Ferguson, David Moyes hakuwa na la maana kwa Zaha zaidi ya kumpuuza na kumsotesha benchi kabla ya baadae mchezaji huyo kupelekwa kwa mkopo Cardiff City na baadae kuuzwa jumla kwa timu yake ya zamani Crystal Palace ambako kwa sasa anang'ara kupita maelezo.

Akizungumzia uvumi wa kutembea na binti wa Moyes, Zaha alisema: "Sikuwahi kutembea na binti wa Moyes, wala sikuwahi kuwa na tabia mbaya.

"Huo ni uvumi ulionitesa hadi nilipoondoka United, sikuwa na la kusema kwa wakati ule. Sikuwahi kuonana hata mara moja na Lauren na sijui ni wapi ulipotokea uvumi ule."
Zaha says that he was                  unhappy at Manchester United and felt isolated by the                  atmosphere at the club
Zaha amefichua kuwa maisha yake ndani Manchester United hayakuwa na furaha
During Zaha's time at                  United, rumours surfaced that he had slept with David                  Moyes's daughter, Lauren
Katika muda wake aliokaa United, Zaha alipakaziwa kuwa ametembea na binti wa Moyes aitwae Lauren (pichani)
The winger says that he                  never met Lauren and does not understand why the rumours                  came about
Zaha anasema hajawahi kukutana na Lauren na hajui tetesi zilitokea wapi
Zaha, playing for United,                  vies for the ball with Wigan's Stephen Crainey in the                  2013 Community ShieldZaha akiichezea United dhidi ya Wigan mwaka 2013 katika Community Shield
Zaha says that he endured a                  distant relationship with former Red Devils boss MoyesZaha anadai hakuwa na uhusiano mzuri na boss wa zamani wa United David Moyes
Zaha was offered little                  explanation behind his first-team exile at United and                  later rejoined Palace  
Zaha hakuwa na amani ndani ya Manchester United
Zaha skips past Manchester                  City defender Eliaquim Mangala (left) during the League                  Cup fourth-round tie
Zaha akimpita beki wa Manchester City  Eliaquim Mangala (kushoto) wakati wa mchezo wa League Cup
Zaha controls the ball ahead                  of Leicester City defender Christian Fuchs at the King                  Power Stadium
Zaha akimiliki mpira mbele ya beki wa Leicester City  Christian Fuchs kwenye uwanja wa King Power 
Zaha scores during the 3-3                  Premier League draw with Newcastle at St James' Park                  last season  
Zaha sakifunga katika mechi ya 3-3 ya Premier League dhidi ya  Newcastle ndani ya St James' Park msimu uliopita
Zaha is relishing the                  positive chemistry he shares with Eagles manager Alan                  Pardew
Zaha akiwa na kocha wake Alan Pardew


Comments