XAVI AMTABIRIA MAKUBWA JACK WILSHERE


XAVI AMTABIRIA MAKUBWA JACK WILSHERE
Wilshere 1
Mkongwe wa Barcelona Xavi Hernandez, anaamini kuwa Jack Wilshere ni moja kati ya wachezaji wa Arsenal na Uingereza wenye ubora wa hali ya juu sana pale tu anapokuwa fiti bila ya kusumbuliwa na majeraha yoyote.
Majeraha ya mara kwa mara yanayomkabili Wilshere yamekuwa yakimpa wakati mgumu sana kuwa katika kiwango bora kwenye misimu mingi, kiasi cha kushindwa kucheza hata mchezo mmoja tangu kuanza kwa msimu mpya wa ligi mwezi Agosti.
Lakini Xavi anasema kwamba Wilshere, ambaye aliposti picha kwenye Twitter akiwa na shati ya Arsenal yenye jina la 'Parlour 11' nyuma na nyingine ikiwa na jina la 'Bergkamp 10', ana uwezo mkubwa unamtofautisha na wachezaji wengi wa Kiingereza wa sasa huku akikumbushia kiwango kikubwa sana alichokionyesha dhidi ya Barcelona katika Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2011.
Jack Wilshere took to Twitter to pose in a                    vintage Arsenal shirt with 'Parlour 11' on the back
Arsenal and England midfielder Wilshere also                    showed off this photo of himself in a Dennis Bergkamp                    shirt 
Wilshere battling with Xavi during the Champions                    League clash between Arsenal and Barcelona in 2011

Madhila ya majeraha kwa WILSHERE

Oktoba 2009 – kifundo cha mguu (nje kwa wiki tano)
Januari 2010 – majeraha ya nyama za paja(wiki tano nje)
Novemba 2010 – Mgongo(nje wiki mbili)
Augosti 2011 – Kifundo cha mguu(miezi 14)
Februari 2013 – Paja(wiki moja nje)
Machi 2013 – Kifundo cha mguu (wiki nne nje)
Mei 2013 – kifundo cha mguu (wiki saba nje)
Oktoba 2013 – Kifundo cha mguu (wiki mbili nje)
Januari 2014 – Kifundo cha mguu (wiki mbili)
Machi 2014 – Kifundo cha mguu (miezi miwili)
Oktoba 2014 – Kifundo cha mguu (wiki mbili)
Novemba 2014 – Kifundo cha mguu (miezi mitano)
Agosti 2015 – Kifundo cha mguu (mpaka sasa yuko nje bado)
 
'Alicheza mpira mkubwa sana dhidi yetu mwaka 2011,' Xavi alisema wakati akiongea na  Sport magazine. Lakini bila ya kusahau alikuwa na umri wa miaka 20 au 21 (alikuwa ana miaka 19). Ni vibaya tu kuona ana majeraha ya mara kwa mara kwa miaka mingi mfululizo.
'Kama ataendelea kuwa kama alivyo atafanya makubwa sana katika klabu ya Arsenal ama timu ya taifa ya Uingereza. Ni mchezaji wa kipekee kabisa katika taifa la Uingereza.
'Hata kama amekuwa akitumia nguvu kwa kiasi fulani lakini ana kipaji cha aina yake, ana uwezo mkubwa wa kupiga pasi na pia uwezo wa kumiliki mpira. Haonekani kama ni mchezaji wa Kiingereza!'


Comments