WAYNE ROONEY, CARRICK NA ASHLEY YOUNG WALIVYOIUA MANCHESTER UNITED NDANI YA OLD TRAFFORD ...Middlesbrough yasonga mbele Capital One Cup



WAYNE ROONEY, CARRICK NA ASHLEY YOUNG WALIVYOIUA MANCHESTER UNITED NDANI YA OLD TRAFFORD ...Middlesbrough yasonga mbele Capital One Cup

Manchester United iliyosheheni wachezaji wake wa kikosi cha kwanza, imeungana na vigogo wengine Arsenal na Chelsea kuiaga michuano ya Capital One Cup baada ya kunyukwa kwa penalti na Middlesbrough.

Mbaya zaidi ni kwamba United imeng'olewa mbele ya mashabiki 70,000 waliofurika kwenye uwanja wao wa nyumbani Old Trafford.

Kikosi cha United kinachanolewa na Louis van Gaal, kililazimishwa sare ya 0-0 katika dakika 120 na hivyo mchezo ukaamuliwa kwa mikwaju ya penalti ambapo wenyeji wakapoteza penalti tatu kupitia kwa wachezaji wake nyota Wayne Rooney, Michael Carrick na Ashley Young.

Kiujumla Middlesbrough ilicheza vizuri zaidi na kustahili kusonga mbele licha ya madai ya United kulalamikia kunyimwa penalti baada ya mpira Daniel Ayala kuunawa mpira ulipigwa na Anthony Martial.

MANCHESTER UNITED (4-3-3): Romero 6.5; Darmian 6, Smalling 6, Blind 5.5, Rojo 6.5 (Young 61 6); Carrick 6, Fellaini 6, Pereira 5.5; Lingard 6, Wilson 5.5 (Rooney 45 6), Depay 5.5 (Martial 70 6)

MIDDLESBROUGH (4-2-3-1): Mejias 7; Kalas 7, Ayala 7.5, Gibson 6.5, Friend 6.5; Stephens 6 (Clayton 114), Leadbitter 6; Nsue 6, Downing 6.5, de Pena 6 (Zuculini 79); Kike 6 (Nugent 84)
Manchester United captain Wayne Rooney has his                  penalty saved by Middlesbrough goalkeeper Tomas Mejias                  in the shootout
Nahodha wa Manchester United  Wayne Rooney akipiga penalti iliyookolewa na kipa wa Middlesbrough  Tomas Mejias 
Boro star Stewart Downing salutes the visiting fans                  after Rooney's spot-kick miss at Old Trafford in the                  Capital One Cup fourth round
 Stewart Downing  wa Middlesbrough (wanne kushoto)  akisalimia mashabiki baada ya Rooney kukosa penalti kwa upande wa United kwenye dimba la  Old Trafford 
Michael Carrick ballooned his effort over the                  crossbar as Championship side Middlesbrough secured a                  famous win on Wednesday night
Michael Carrick akigonga mwamba na kuikosesha United penalti
Ashley Young completed a hat-trick of England                  international's missing spot-kicks as Mejias saved the                  decisive penalty
Ashley Young akikosa penalti ya tatu kwa upande wa United
The Boro players rush to congratulate Mejias, their                  hero at Old Trafford after saving two penalties                  following a goalless 120 minutes
Middlesbrough wakishangilia ndani ya Old Trafford
Ben Gibson and his Middlesbrough team-mates                  celebrate in front of the travelling faithful as they                  booked their place in the quarter-finals
Ben Gibson na wachezaji wenzake wa Middlesbrough wakishangilia baada ya kufuzu kwenda hatua ya robo fainali ya Capital One kwa kuing'oa Manchester United
The Manchester United stars look dejected after                  they were dumped out of the Capital One Cup on Wednesday                  night
Wachezaji wa Manchester United wanavyoonekana baada ya kutupwa nje kwenye michuano ya Capital One Cup Jumatano usiku
United boss Louis van Gaal will have rebuild his                  side's morale ahead of their trip to Crystal Palace in                  the Premier League on Saturday
Kocha wa United  Louis van Gaal akiwa na msaidizi wake Ryan Giggs kwenye mchezo wa Capital One







Comments