SIR ALEX FERGUSON ASEMA RYAN GIGGS ALISTAHILI KUWA MRITHI WAKE MANCHESTER UNITED


SIR ALEX FERGUSON ASEMA RYAN GIGGS ALISTAHILI KUWA MRITHI WAKE MANCHESTER UNITED
Sir Alex Ferguson amekiri kuwa Ryan Giggs angeweza kuwa mrithi wake kama angestaafu kusakata kabumbu wakati akiwa na umri wa miaka 35.
Giggs ambaye kwa sasa ni msaidizi wa Louis van Gaal,  alitundika daluga akiwa na umri wa miaka 40 huku mchezo wake wa mwisho ukiwa ni dhidi ya Hull City mwezi Mei mwaka 2014.
Ferguson amesema: "Kama Ryan Giggs angestaafu miaka sita au saba iliyopita, basi huenda muda angekuwa kocha mkuu wa Manchester United.
"Hakuna ubishi, kama angestaafu akiwa na umri wa miaka 35, ningemfanya msaidizi wangu na hiyo ingempa nafasi ya kuchukua moja kwa moja nafasi yangu pale nilipostaafu.
"Angepata uzoefu mkubwa chini yangu kama anaoupata kwa Luis van Gaal hivi sasa. Hata hivyo sikuwahi kumwomba atundike daluga." 
Ryan Giggs (right) is                  currently assistant to Manchester United manager Louis                  van Gaal (left) at Old Trafford
Ryan Giggs (kulia) kwa sasa ni kocha msaidizi  Manchester United chini ya Louis van Gaal (kushoto) 
Sir Alex Ferguson admits                  Giggs could have succeeded him as United manager had he                  retired at the age of 35
Sir Alex Ferguson amekiri kuwa Giggs angeweza kuwa mrithi wake



Comments