RAFA BENITEZ AANZA KUONJA JOTO YA JIWE KWA MASUPASTAA WA REAL MADRID ...Sergio Ramos amtolea uvivu



RAFA BENITEZ AANZA KUONJA JOTO YA JIWE KWA MASUPASTAA WA REAL MADRID ...Sergio Ramos amtolea uvivu
Nguvu ya wachezaji masupastaa Real Madrid huenda ikamtafuna kocha Rafa Benitez, hiyo ni baada ya nahodha Sergio Ramos kujibu mapigo ya shutuma za kocha huyo.

Benitez alishmtumu hadharani Ramos baada ya mchezo dhidi ya mahasimu wao Atletico Madrid na kusema nahodha huyo alipoteza mpira kizembe kipindi cha kwanza ambapo katika juhudi zake za kuukomboa mpira alioupoteza, akacheza rafu iliyosababisha penalti.

"Kilichonishangaza ni kosa la Ramos alipoporwa mpira kwa kufanya masihara kwenye eneo hatarishi," alisema kocha huyo katika mazungumzo yake na vyombo vya habari.

Ramos akajibu mapigo  siku mbili baadae akiwa na timu ya taifa ya Hispania kwa kusema: "Tungeweza kuzungumza kuhusu makosa yangu au tungeweza pia kuzungumzia makosa yetu ya kubadilisha wachezaji (substitutions) katika mchezo. Wote tunajifunga kutokana na makosa, wachezaji na makocha."

Beki huyo alikuwa analenga 'sub' iliyofanywa na Benitez ya kumtoa mfungaji wa bao la Real Madrid Karim Benzima ambayo alidai ilichangia kuigharimu timu.

Kauli hiyo ya Ramos Ilikuwa ni kama angalizo tosha kwa Benitez - ukinilipua hadharani na mimi ntakulipua hadharani.

Real Madrid manager Rafa                  Benitez called Sergio Ramos to explain his recent                  post-match comments
Sergio Ramos akwazana na kocha wake
Benitez openly criticised                  Ramos after the Spain international gave the ball away                  ahead of Atletico's equaliser
Benitez alimshutumu Ramos hadharani kwa kusababisha goli la kusawazisha la Atletico Madrid
Ramos hit back at Benitez                  while on international duty by questioning the Real                  manager's substitutions
Ramos nae akajibu mapigo kwa Benitez 


Comments