NEWCASTLE YAONA MWEZI, YAPATA USHINDI WA KWANZA PREMIER LEAGUE ...yainyuka Norwich 6-2



NEWCASTLE YAONA MWEZI, YAPATA USHINDI WA KWANZA PREMIER LEAGUE ...yainyuka Norwich 6-2
Georginio Wijnaldum amefunga magoli manne kati ya sita yaliyoipa ushindi wa kwanza Newcastle kwenye Premier League dhidi ya Norwich.

Katika mchezo huo uliomalizika kwa matokeo ya 6-2, Georginio Wijnaldum alifunga katika dakika ya 14, 26, 65, 85 huku magoli mengine yakifungwa na Ayoze Perez dakika ya 33 na Aleksandar Mitrovic kunako dakika ya  64 wakati yale ya Norwich yaliwekwa kimiani na Dieumerci Mbokani dakika ya 20 na  Nathan Redmond dakika ya 35.

Ushindi huo wa Newcastle umekuwa ni ahueni kwa kocha 

Steve McClaren ambaye kibarua chake kipo hatarini kutokana na mwenendo mbaya wa timu yake.


NEWCASTLE UNITED (4-4-2): Elliot 6; Janmaat 6, Mbemba 6, Coloccini 6, Dummet 6 (Haidara 64mins 6); Sissoko 7.5, Colback 7, Tiote 6.5 (Anita 45mins 6.5), Wijnaldum 8;Perez 7, Mitrovic 7 (Cisse 86mins 6).

NORWICH CITY (4-2-3-1): Ruddy 5.5; Whittaker 6, Martin 5.5, Bassong 5.5, Olsson 6 (Jerome 83mins 6); Dorrans 6 (O'Neill 83mins 6), Tettey 6 (Hoolahan 61mins 6); Redmond 7, Howson 6, Brady 6; Mbokani 7.
Georginio Wijnaldum amefunga mara nne dhidi ya Norwich wakati  Newcastle ikishinda 6-2 
Wijnaldum celebrates                  alongside his Newcastle team-mates after scoring four                  goals in their 6-2 victory against Norwich
Wijnaldum akishangilia moja ya magoli yake
Wijnaldum fired Newcastle                  into the lead against Norwich in the Premier League                  encounter at St James' Park
Wijnaldum akiifungia Newcastle bao la kwanza kwenye dimba la  St James' Park




Comments