DJIBRIL CISSE AANGUSHA KILIO WAKATI AKITANGAZA KUSTAAFU SOKA



DJIBRIL CISSE AANGUSHA KILIO WAKATI AKITANGAZA KUSTAAFU SOKA
Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Sunderland na Queens Park Rangers za England,  Djibril Cisse ametangaza kustaafu soka na kuangusha kilio kupitia matangazo yaliyokuwa yakirushwa 'live' na televisheni ya Ufarsansa.



DJIBRIL CISSE'S CLUB CAREER

Auxerre                         166 games (90 goals)
Liverpool                          83 (24)
Marseille (loan)                25 (15)
Marseille                          53 (22) 
Sunderland (loan)            38 (11)
Panathanikos                   89 (55)
Lazio                                27 (5)
QPR                                 29 (10)
Al-Gharafa (loan)            17 (5)
Kuban Krasnodar            25 (5)
Bastia                              25 (6)
Cisse ambaye amechezea timu ya taifa ya Ufaransa mara 41 pamoja na vilabu 12 ndani ya miaka 15, ameamua kustaafu baada kucheza kwa zaidi ya mwaka mmoja bila kufunga hata goli moja la ligi.

Mshambuliaji huyo mtukutu akashindwa kuyazuia machozi yake wakati kocha wake wa zamani Guy Roux alipokuwa akizungumza machache ya kumsifia.

Cisse mshindi wa Champions League akiwa na Liverpool, aliyetwaa kiatu cha dhahabu mara mbili Ufaransa na Ugiriki, alitumikia miaka mitano kusakata kabumbu ndani ya England ambapo alizichezea Liverpool aliyoifungia magoli 24, Sunderland na Queens Park Rangers.

Licha ya kutikisa nyavu mara 250 kwa nchi yake na vilabu, lakini hakufunga hata goli moja la ligi kuu  msimu uliopita ingawa aliifungia klabu yake mabao matatu kwenye michuano mingine.

Cisse alianza soka lake kwenye klabu Auxerre wakati kocha Roux alipompa nafasi kwenye kikosi cha kwanza akitokea kwenye academy ya timu hiyo.

Former Liverpool striker                  Djibril Cisse broke down on live TV after announcing his                  retirement from football
 Djibril Cisse akilia wakati alipokuwa anatangaza kustaafu soka
Cisse holds back the tears                  after bringing his career to an end, following 15 years                  at the top around the world
Cisse akipambana kuyazuia machozi
The striker spent the last                  two seasons at Bastia, but hasn't scored a league goal                  since April 2014
Cisse alitumia misimu miwili iliyopita akiwa na Bastia lakini hakuweza kufunga hata goli moja la ligi tangu April 2014
Cisse is best remembered in                  England for his time at Liverpool, where he scored 24                  goals in two seasons
Cisse atakumbukwa vizuri katika muda wake alioitumikia Liverpool na kufunga magoli 24 ndani ya misimu miwili
The French forward won the                  Champions League with Liverpool in their famous victory                  over AC MIlan in 2005
Hapa Cisse akiwa na medali ya Champions League baada ya Liverpool kuishinda AC MIlan mwaka 2005




Comments