DEAL DONE, BADO UTAMBULISHO RASMI TU…


DEAL DONE, BADO UTAMBULISHO RASMI TU…

LIVERPOOL, ENGLAND - OCTOBER 08: (THE SUN OUT, THE SUN              ON SUNDAY OUT) (MINIMUM PRINT FEE OF GBP 250, BROADCAST FEE              OF GBP 150, ONLINE FEE OF GBP 100 PER IMAGE, OR LOCAL              EQUIVALENT) (EDITORS NOTE: Image background must not be              altered) (EXCLUSIVE COVERAGE) New Manager of Liverpool              Jurgen Klopp signs his new contract to manage Liverpool with              Ian Ayre chief executive officer of Liverpool Football on              October 8, 2015 in Liverpool, England. (Photo by Andrew              Powell/Liverpool FC via Getty Images)

Mjerumani Jurgen Klopp anakabiliwa na mtihani wa kuirudisha Liverpool katika chati yake ya kuwa tishio ulaya baada ya kusaini mkataba wa kukinoa kikosi hicho kwa misimu mitatu.

Kocha huyo amembadili Brendan Rodgers aliyekua akikinoa kikosi hicho bila ya mafanikio kwa misimu miwili iliyopita na hatimaye kufukuzwa juma lililopita.

Klopp ambaye alijiuzulu kuifundisha Borrusia Dortmund msimu uliopita anatarajiwa kutambulishwa leo kwa vyombo vya habari mara baada ya kusaini mkataba jana Alhamisi.

Katika hali isiyo ya kawaida, klabu ya Borrusia Dortmund kupitia ukurasa wake wa Twitter imemtakia kila la kheri kocha huyo katika maisha yake mapya na Liverpool.

Dortmund walipost picha ya mjerumani huyo huku wakimtakia kila lenye heri. Liverpool nao waliwajibu wenzao wa Dortmund kwa furaha waliyokua nayo kwa kupokea ujumbe huo.

Kocha huyo sasa ataanza mtihani wake wa kwanza dhidi ya Tottenham Hotspur weekend ijayo katika mchezo wa ligi kuu England ugenini White Hart Lane.



Comments