BRENDAN RODGERS KAPATA KAZI HII MPYA.


BRENDAN RODGERS KAPATA KAZI HII MPYA.

rod
Ukishafanya kazi ya kuiongoza taasisi kubwa kama Liverpool mambo yako hayawezi kuwa mabaya hata kama umeachishwa kazi. Hivyo ndivyo imemtokea Brendan Rodgers ambae siku kadhaa zilizopita alifukuzwa kazi na club ya Liverpool na sasa hivi taarifa zimetoka kwamba ameshapata kazi mpya.

Kazi ya ukocha kwa sasa sio rahisi kwasababu club zote ndio kwanza zimeanza ligi na makocha wao. Kazi aliyopata Brendan Rodgers ni ya kuwa mchambuzi kwenye TV ya beIN Sports ya huko Qatar.

Rodgers anategemewa kuwa mmoja kati ya wachangiaji wa mechi za EPL ambazo zinaonyeshwa na channel hiyo aki ripoti kutoka kwenye studio zao huko Qatar. Mambo sio mabaya kwa Rodgers kwasababu warabu huwa hawana tabu kwenye swala la kuweka mzigo mzito kwa ajili ya watu wanaofanya kazi zao.



Comments