BARCELONA, REAL MADRID, BAYERN ZAFANYA KUFURU TUZO YA MWANASOKA BORA DUNIANI (Ballon d'Or) ...MAN CITY YAJIKAKAMUA, ARSENAL, CHELSEA ZAAMBULIA NAFASI MOJA, MAN UNITED YATOKA MIKONO MITUPU




BARCELONA, REAL MADRID, BAYERN ZAFANYA KUFURU TUZO YA MWANASOKA BORA DUNIANI (Ballon d'Or) ...MAN CITY YAJIKAKAMUA, ARSENAL, CHELSEA ZAAMBULIA NAFASI MOJA, MAN UNITED YATOKA MIKONO MITUPU
Winga wa Wales  Gareth Bale ndiye mchezaji pekee kutoka Uingereza aliyejumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji 23 watakaowania tuzo ya mwanazoka bora duniani - Ballon d'Or, akiwa ameingia kwenye orodha hiyo kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Bale ni miongoni mwa wachezaji 11 kutoka ligi kuu ya Hispania (La Liga) wanaowania tuzo hiyo huku Premier League na Bundesliga zikiwa zimetoa wachezaji watano kila moja.

Manchester City ya England imeingiza wachezaji watatu Sergio Aguero, Kevin De Bruyne na Yaya Toure huku Chelsea ikiambulia mchezaji mmoja Eden Hazard.

Arsenal pia imefanikiwa kupata nafasi moja kupitia kwa Alexis Sanchez wakati Manchester United, Liverpool na vilabu vingine vya England vikitoka patupu.

Kwa mara nyingine tena Real Madrid na Barcelona zimetawala kwenye orodha hiyo itakayotoa mchezaji bora wa dunia Januari 11, 2016 huko Zurich.

Bale anaungana na mshindi wa mwaka 2014 Cristiano Ronaldo,  Karim Benzema, Toni Kroos na  James Rodriguez katika jumla ya wachezaji watano wa Real Madrid walioingia kwenye orodha ya Ballon d'Or, wakati Lionel Messi akiwa na Neymar, Luis Suarez, Javier Mascherano, Andres Iniesta na Ivan Rakitic kwa upande wa Barcelona yenye wachezaji sita.

Bayern Munich nayo imeingiza wakali watano Robert Lewandowski, Thomas Muller, Manuel Neuer, Arjen Robben na  Arturo Vidal, huku Paul Pogba wa Juventus na  Zlatan Ibrahimovic wa Paris Saint-Germain wakikamilisha orodha hiyo.

Arsene Wenger na Jose Mourinho ni miongoni mwa makocha 10 wanaowania tuzo ya kocha bora wa mwaka sambamba na Luis Enrique wa Barcelona na  Pep Guardiola wa Bayern Munich.

Makocha wengine ni  Massimiliano Allegri wa Juventus, Unai Emery wa Sevilla, Laurent Blanc wa PSG,  Diego Simeone wa Atletico Madrid na Carlo Ancelotti aliyetimuliwa Real Madrid kiangazi kilichopita, wakati kocha wa Chile Jorge Sampaoli naye ameingia kwenye orodha hiyo.
Real Madrid forward Gareth                  Bale is the only British player to be on the Ballon d'Or                  shortlist 
Mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale (kulia) ni Mwingereza pekee kwenye orodha ya wachezji wanaowania Ballon d'Or 
Cristiano Ronaldo is another                  Real Madrid player who is on the 23-man shortlist for                  the awardCristiano Ronaldo (kushoto) mchezaji mwingine wa Real Madrid katika orodha ya wanasoka 23 wanaowania Ballon d'Or 
Barcelona due Lionel Messi                  and Neymar are also in the running for the Ballon d'Or
Mastaa wa BarcelonaLionel Messi na  Neymar nao wamo
Manchester City star Sergio                  Aguero is one of five representatives from the Premier                  League on the list 
Mshambuliaji wa Manchester City  Sergio Aguero ni mmoja wa wachezaji watano wa Premier League waliojumuishwa kwenye list ya Ballon d'Or 
Alexis Sanchez of Arsenal is                  another Premier League player who is on the Ballon d'Or                  shortlist
Alexis Sanchez wa  Arsenal (katikati) nyota mwingine wa Premier Legue kwenye kimbembe cha Ballon d'Or 
Chelsea boss Jose Mourinho                  is on the shortlist for coach of the year 
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho anawania nafasi ya Kocha bora wa mwaka duniani
England boss Mark Sampson is                  on the coach of the year for women's football shortlistKocha wa soka la wanawake wa England Mark Sampson anatajwa miongoni mwa makocha wanaowania nafasi ya kocha bora wa soka la wanawake

ORODHA WA YA WACHEZAJI BORA NA MAKOCHA BORA

BALLON D'OR SHORTLIST: Sergio Aguero (Argentina/Manchester City), Gareth Bale (Wales/Real Madrid), Karim Benzema (France/Real Madrid), Cristiano Ronaldo (Portugal/Real Madrid), Kevin De Bruyne (Belgium/Manchester City), Eden Hazard (Belgium/Chelsea), Zlatan Ibrahimovic (Sweden/Paris St Germain), Andres Iniesta (Spain/Barcelona), Toni Kroos (Germany/Real Madrid), Robert Lewandowski (Poland/Bayern Munich), Javier Mascherano (Argentina/Barcelona), Lionel Messi (Argentina/Barcelona), Thomas Muller (Germany/Bayern Munich), Manuel Neuer (Germany/Bayern Munich), Neymar (Brazil/Barcelona), Paul Pogba (France/Juventus), Ivan Rakitic (Croatia/Barcelona), Arjen Robben (Holland/Bayern Munich), James Rodriguez (Colombia/Real Madrid), Alexis Sanchez (Chile/Arsenal), Luis Suarez (Uruguay/Barcelona), Yaya Toure (Ivory Coast/Manchester City), Arturo Vidal (Chile/Bayern Munich).
COACH OF THE YEAR SHORTLIST: Massimiliano Allegri (Juventus), Carlo Ancelotti (Formerly of Real Madrid), Laurent Blanc (Paris St Germain), Unai Emery (Sevilla), Pep Guardiola (Bayern Munich), Luis Enrique (Barcelona), Jose Mourinho (Chelsea), Jorge Sampaoli (Chile), Diego Simeone (Atletico Madrid), Arsene Wenger (Arsenal).



Comments