BARCELONA KUISHANGAZA DUNIA KWA USAJILI WA ROBIN VAN PERSIE.


BARCELONA KUISHANGAZA DUNIA KWA USAJILI WA ROBIN VAN PERSIE.

2D70766F00000578-0-image-a-8_1444908771167

Ilionekana kwamba Van Persie yupo kwenye siku zake za mwisho kwenye soka na akahamia club ya Fenerbahce akitokea Manchester united. Sasa habari mpya ni kwamba Van Persie anatakiwa kujiunga na club ya Barcelona ikifika mwezi wa kwanza 2016.

Barcelona wanatafuta foward mwingine atakayekua back up wa wachezaji watatu Neymar, Messi na Suarez. Combination ya hawa watatu imeonekana kulegea baada ya Messi kuwa nje ya uwanja na hakuna mchezaji mwigine anaekamilisha hiyo crew ya wachezaji watatu kama Barcelona ilivyozoea kucheza.

Van Persie ambae yupo Fenerbahce anaweza kuwa nafasi ya kuhamia Barcelona kama inayo ripotiwa sasa hivi kutokana na kutokua na maelewano mazuri na kocha wake. Kutokuelewana huko inatokana na kwasababu Van Persie anatupia mara chache sana nyavuni kama ilivyotegemewa.

Barcelona wanahitaji kuwa na uhakika na kikosi chao kwa sababu wapo kwenye vita ya kutetea makombe makubwa ambayo waliyashinda kwenye msimu uliopita.



Comments