BALAA FIFA! Sepp Blatter na Michel Platini kusimamishwa kazi kwa siku 90



BALAA FIFA! Sepp Blatter na Michel Platini kusimamishwa kazi kwa siku 90
Kamati ya maadili katika shirikisho la soka duniani FIFA imependekeza Rais wa shirikisho la soka duniani FIFA  Sepp Blatter asimamishwe kazi kwa siku tisini.
Kamati hiyo pia imependekeza hatua kama hiyo ichukuliwe kwa rais wa UEFA Michel Platini.
Wanachama wa kamati hiyo walikutana wiki hii baada ya Jaji mkuu nchini Uswizi kufungua mashtaka ya uhalifu dhidi ya Blatter mwezi uliopita.
Blatter anatuhumiwa kwa kutia saini kandarasi zisizo na manufaa yoyote kwa FIFA mbali na kufanya 'malipo' kwa rais wa shirikisho la UEFA Michel Platini.
Blatter ambaye ni raia wa Uswizi amekuwa rais wa FIFA tangu mwaka 1998.
Michel Platini amekuwa akitajwa kama mtu mwenye nafasi kubwa ya  kumrithi Blatter na iwapa pendekezo hili litapitishwa, basi ndoto yake ya kuwa rais wa FIFA itayeyuka.


Comments