Watu 13 wamepoteza maisha yao baada ya mtumbwi            walimokuwa wakisafiria kugongana na feri Idara ya kulinda            fukwe za bahari ya Uturuki imetangaza.
        13 wanadhaniwa kuwa ni wahamiaji.
        Mtumbwi huo unaaminika kuwa ulikuwa ukielekea katika            kisiwa cha Lesbos kilichoko ugiriki ajali hiyo ilipotokea.
        Ajali yenyewe imetokea karibu na bandari ya Canakkale            Uturuki.
        Kwa mujibu wa shirika la habari la Dogan mtumbwi huo            ulikuwa na jumla ya watu 46.
        20 kati yao waliokolewa majini huku wengine 13 wakiwa            hawajapatikana.
        4 kati ya wale waliokufa maji ni watoto.
        Wakati huohuo idadi kubwa ya wahamiaji wanazidi            kuelekea katika mataifa ya bara ulaya.
        Foleni kubwa ya watu imeripotiwa kwenye mpaka kati ya            Slovenia Austria na Croatia licha ya mikakati ya kuwazuia            kuingia katika mataifa hayo.
        Kuwepo kwao katika eneo hilo la Ulaya kumezua            makabiliano baina ya Austria, Hungary na Croatia.
        
Comments
Post a Comment