Siku za utawala wa kocha Brendan Rogers ndani ya klabu ya          Liverpool zimeanza kuhesabika baada ya mfululizo wa matokeo          wanayopata Liverpool katika siku za hivi karibuni .
Liverpool mabingwa wa mara 18 wa ligi kuu ya England, waliendelea kuusotea ubingwa huo ambao mara ya mwisho kuuchukua miaka ni takribani 20 iliyopita, msimu uliopita walimaliza nje ya Top 4 na hivyo kukosa nafasi ya kushiriki katika michuano ya Champions League pamoja kufanya uwekezaji mkubwa katika usajili.
Msimu huu pia wameuanza vibaya pamoja na kuwekeza fedha nyingi kwenye usajili, wamecheza mechi 7, wakishinda 3, sare 2, na wakipoteza 2 – ukiwemo mchezo dhidi ya mahasimu wao Manchester United. Na baada ya mchezo watu wameanza kuishinikiza bodi kumtimua kazi. Lakini yote yametokana na mambo manne yafuatayo:
1) USAFIRI
  Moja ya matatizo makuu yanayoisumbua Liverpool          ni usajili wa wachezaji wanaofanya. Rodgers amefanya usajili wa          wachezaji wengi sana na wengi wao aidha amewatoa kwa mkopo au          kawauza. Hajafanya usajili mzuri pamoja bajeti nzuri anayopewa.          Mamilioni ya paundi yametumika kwa wachezaji ambao wameshindwa          kuipa Liverpool ubora inaohuhitaji na ndio maana timu chini ya          Rogers haijaweza kuendelea kwa mafanikio.
          2) Matatizo katika Safu ya Ulinzi
  Liverpool wamekuwa na kiwango kibovu katika          ulinzi katika miaka ya hivi karibuni. Safu ya ulinzi          iliwagharimu ubingwa miaka miwili iliyopita- walikuwa na safu          kali mno ya ushambuliaji lakini beki dhaifu. Waliruhusu magoli          mengi mno. Usajili uliofuatia baada ya hapo hakusaidia pia.          Dejan Lovren ameendelea ku-flop kila msimu na Sakho amekuwa          usajili wa ghali ukilinganisha na mchango wake kwenye timu.          Kimuundo Liverpool wapo wazi nyuma na wameruhusu magoli mengi          msimu huu. Rogers amekuwa akibadili mfumo kwa kucheza na mabeki          wanne au watatu na hilo halijaweza kuwa tiba. Muundo wa safu ya          ulinzi haupo sawa.
          3) Matatizo kwenye Ushambuliaji 
  
          Luis Suarez alikuwa sababu kubwa ya kwanini Liverpool          walifanikiwa kumaliza katika nafasi ya pili miaka miwili          iliyopita. Alifunika matatizo mengi katika timu hiyo na kwa          hakika alikuwa 'world class talent', akiwa ndio mchezaji bora          katika ligi. Kwa namna ya kipekee aliibeba Liverpool na          kuisogeza kabisa katika ndoto ya kutwaa ubingwa. Alipoondoka,          matatizo aliyokuwa akiyafunika yaliyoonekana wazi. Liverpool          mpaka sasa hawajaweza kumsaini mchezaji mwenye uwezo wa kuwa          mbadala wa Suarez, na sasa Christian Benteke ndio mchezaji mpya          aliyesajiliwa kwa fedha nyingi kuziba pengo la Suarez.
Majeruhi kwa Daniel Sturidge yamezidi kukuza tatizo, kwa sababu          amekuwa muhimu katika kuisadia timu. Msimu kabla ya mechi          wikiendi iliyopita walikuwa wamefunga magoli manne tu katika          mechi 6.
          4) Filosofi Isiyoeleweka
  
          Rodgers anajiona kama kocha mwenye filosofia ya kiufundi          inayoeleweka. Akiwa Swansea – timu ilikuwa ikicheza soka safi          huku ikitawala mchezo  na walipata sifa kubwa kwa aina hiyo ya          mchezo. Alipokuja Liverpool, walikuwa na kasi huku wakitawala          mpira, mchezo uliopelekea kushindani ubingwa lakini tangu wakati          huo hana filosofia ya ufundi inayoeleweka. Amekuwa akitumia          mifumo mingi na akiwapanga wachezaji katika nafasi wasizozimudu,          mfano Danny Ings akicheza kama winga au Markovic akicheza kama          wing-back – mifumo hii imeharibu kuboreka kwa kikosi na          kutokuonyesha kiuhalisia nini anataka kufanya. Kwa usajili wote          aliofanya bado haipo wazi mchezaji gani anafiti kucheza sehemu          gani na kwanini. Matatizo yote haya yanazalishwa na kutokuwa na          sera nzuri ya usajili ambayo inamfanya asionekane kuwa na          filosofia yenye kueleweka.
Comments
Post a Comment