Carlos Tevez ameomba radhi baada ya kumvunja mguu                kiungo wa Argentinos                Juniors Ezequiel Ham wakati Boca Juniors                ikishinda 3-1 Jumamosi usiku.
        Mshambuliaji huyo wa zamani wa Juventus alifunga                mara mbili katika mchezo huo lakini mchango wake huo                ukafunikwa na tukio la simanzi pale alipomvunja Ezequiel Ham katika juhudi ya                kupora mpira.
        Tevez              mwenye umri wa miaka 31 akasema baada ya mchezo huo:              "Imeniuma sana kwa sababu nilikuwa nafuata mpira,              sikukusudia kumuumiza, baada ya miguu yetu kukugusana              nikajua nimefanya kitu cha hatari,"
        Carlos Tevez akimpeleka              mguu wake kwenye mguu wa Ezequiel Ham na kumsababishia ajali              mbaya
        
Comments
Post a Comment