IMEBAINIKA kuwa, huenda Kocha wa zamani wa Manchester            United, Sir Alex Ferguson angeendelea kuinoa klabu hiyo kama            kusingetokea kifo cha mdogo wa mke wake.
        Ferguson (73), alistaafu mwaka 2013 akishinda mataji 13            ya Ligi Kuu ya Engoland (EPL) akiwa na klabu hiyo.
        Manchester United imeendelea kuwa katika hali ngumu            tangu alipoachiwa mikoba David Moyes na sasa Louis van Gaal.
        Moyes alitimuliwa miezi 10 baadaye, baada ya kushindwa            kutwaa taji la EPL.
        Ferguson alisema kuwa, kifo cha Cathy Ferguson mwaka            2012 kilibadilisha kila kitu katika familia yake.
        Kocha huyo alisisitiza kuwa ilikuwa vigumu kuendelea            kufanya kazi Old Trafford  kwani familia hiyo ilimtaka astafu            tangu mwaka 2002.
        Aidha kocha huyo yupo mbio kuzindua kitabu chake kipya            'Art of Management' kikitokana na uzoefu wake katika soka            akiwamo mchezaji Cristiano Ronaldo ambaye aliitumikia klabu            hiyo mwaka 2003-2009.
                                        
Comments
Post a Comment