Yanga ambayo haijaifunga Simba tangu mwaka 2013,            imeibuka shujaa katika mechi ya watani wa jadi kwa kuibuka na            ushindi wa bao 2-0.
        Katika mchezo huo wa Ligi Kuu uliochezwa uwanja wa            Taifa jijini Dar es Salaam, Simba ilitawala mchezo kwa kiasi            kikubwa lakini Yanga wakawa makini kutumia nafasi chache            walizozipata.
        Balimi Busungu aliyeingia katikati ya kipindi cha            kwanza kuchukua nafasi ya Simon Msuva, ndiye aliyebadili sura            ya mchezo kwa kuchangia bao la kwanza lililofungwa na Amis            Tambwe dakika ya 45.
        Kama vile hiyo haitoshi, Busungu akapachika bao la pili            kipindi cha pili akitumia vizuri makosa ya mabeki wa Simba.
        Mchezo huo ulitawaliwa na kadi nyingi za njano ambazo            zilipelekea Mbuyu Twitte  kulambwa kadi nyekundu dakika ya mwisho wa mchezo.
        
Comments
Post a Comment