MCHEZAJI                namba moja wa zamani katika medani ya tenisi duniani Maria                Sharapova anatarajiwa kurudi katika uga wa mchezo huo                kwenye michuano ya wazi ya Wuhan Open itakayoanza Septemba                27 mwaka huu.
          Michuano hiyo itakayochezwa nchini China itamrudisha              nyota huyo dimbani baada ya kupata maumivu ya goti              yaliyomfanya akose Wimbledon na US Open mwaka huu.
          Sharapova,28, raia wa Russia na bingwa              mara tano wa Grand Slam alikaririwa akisema "Ni wakati              muhimu kwangu kurudi tena katika Michuano ya Wazi ya Wuhan              kwani nimekuwa nikifanya mazoezi kwa bidii kwa ajili ya              kurudi dimbani nikiwa fiti," alisema nyota huyo.
          
Comments
Post a Comment