OSTADH: “MWAKANI TUNAKUJA KIVINGINE…”



OSTADH: "MWAKANI TUNAKUJA KIVINGINE…"
Kiongozi wa kikundi cha ushangiliaji cha Kauzu FC Ally              Juma 'Ostadh' akizungumza mara baada ya kupokea zawadi ya              kikundi bora cha ushangiliaji

Kiongozi wa kikundi cha ushangiliaji cha Kauzu FC  Juma Ally 'Ostadh' akizungumza mara baada ya kupokea zawadi ya kikundi bora cha ushangiliaji

Kiongozi wa kikundi cha ushangiliaji cha timu ya Kauzu FC Juma Ally maarufu kama 'Ostadh' amewashukuru wadhamini wa michuano hiyo baada ya kupokea shilingi milioni moja (1,000,000) kama zawadi ya kikundi bora cha ushangiliaji na kuahidi kuwa wanajipanga kwa ajili ya michuano ya msimu ujao ambayo.

"Nashukuru sana kupata zawadi hii ya ushangiliaji bora na najua kwamba pesa hii si ya kwangu pekeangu bali ni ya kundi zima, ntakachokifanya ni kwenda kuwaambia wenzangu kwamba tumepata zawadi ya kikundi bora cha ushangiliaji na msimu ujao tujipange vizuri zaidi ya mwaka huu", Ostadh alishukuru.

Juma Ally (katikati) akipokea shilingi milioni moja              toka kwa Yahaya (kulia) Mohamed huku Shaffih Dauda (kushoto)              na Daudi Kanuti (nyuma) wakishuhudia

Juma Ally (katikati) akipokea shilingi milioni moja toka kwa Yahaya (kulia) Mohamed huku Shaffih Dauda (kushoto) na Daudi Kanuti (nyuma) wakishuhudia

"Pesa hii tutachua semu kidogo kwa ajili ya kupongezana halafu nyingine tunakwenda kuifungulia account kwasababu mwakani kama Mungu akipenda tutashiriki tena kwa hiyo itakuwa ikitusaidia kwa kununulia vifaa vinavyohitajika kwa ajili ya kikundi cha ushangiliaji".



Comments