NI MIAKA MINNE TOKA KIFO CHA KASALOO KYANGA


NI MIAKA MINNE TOKA KIFO CHA KASALOO KYANGA

LEO ni miaka minne toka kifo cha mmoja wa watunzi na waimbaji bora waliowahi kutokea kataika muziki wa dansi Tanzania, Selemani Kasaloo Kyanga ambae alizikwa katika makaburi ya Sinza . Kasaloo alikuwa ni pacha wa nduguye Kyanga Songa ambae nae ni marehemu, walizaliwa nchini Kongo 1957. Mapacha hawa waliofanana walikuwa nyota katika kila bendi waliyopigia, kati ya bendi walizopigia wakiwa nchini ni Matimila, Makassy, Maquis, Sambulumaa, Ngorongoro Heroes, Tancut Almasi, Kalunde Band na Sandton Sound. Kasaloo atakumbukwa katika nyimbo nyingi zinazoendelea kutamba mpaka leo kama vile Kalubandika, Masafa Marefu, Nimemkaribisha nyoka

Mungu Amlaze pema Seleman Kasaloo Kyanga (Mwanakaa).

299538_2409806803472_36228140_n

Kasaloo akiwa Super matimila

304569_2409806603467_2123275927_n

Kasaloo akisalimiana na marehemu Capt John Komba

317408_2409808683519_381418549_n

Kasaloo akiwa na John Kitime wakipiga wimbo Masafa Marefu

318716_2409808563516_484848602_n

Kasaloo akiwa Tancut Almasi, toka kushoto Buhero Bakari,Abdul Salvador, Kasaloo, Asha Salvador, Kyanga Songa

320151_2409807483489_550525494_n

Kasaloo na Deo Mwanambilimbi wa Kalunde Band

297156_2409807963501_963048663_n

Selema Kasaloo Kyanga

300060_2409806243458_565669702_n 321084_2409807763496_379816835_n



Comments