MOURINHO ASEMA CHELSEA BILA THIBAUT COURTOIS INAWEZEKANA …adai Asmir Begovic ataziba pengo



MOURINHO ASEMA CHELSEA BILA THIBAUT COURTOIS INAWEZEKANA …adai Asmir Begovic ataziba pengo
Chelsea have suffered another                setback after their stuttering start to the defence of                their Premier League title
Jose Mourinho amethibitisha kuwa mlinda mlango namba moja Thibaut Courtois atafanyiwa upasuaji wa goti  na atakuwa nje ya dimba kwa muda mrefu.

Thibaut Courtois aliumia goti akiwa mazoezini mapema wiki hii na sasa Chelsea itaanza kukosa huduma yake kuanzia mechi ya Jumamosi hii dhidi ya Everton.

Hata hivyo Mourinho amejipa moyo na kusema kipa  Asmir Begovic aliyesajiliwa kutoka Stoke City kiangazi hiki, ataziba pengo hilo bila wasiwasi.

Mourinho amesema: "Kila mtu alirejea salama kutoka kwenye mechi za kimataifa, lakini Courtois  akaumia mazoezini na atakosekana kwa muda mrefu."
Jose Mourinho                  confirmed Thibaut Courtois will undergo surgery and he                  will be out for 'quite a long time'
Jose Mourinho akithibitisha kuwa  Thibaut Courtois atakuwa benchi kwa muda mrefu





Comments