MANCHESTER UNITED YAONGOZA LIGI KUU KWA MARA YA KWANZA TANGU SIR ALEX FERGUSON AACHIE NGAZI ...Rooney afunga goli lake la kwanza Premier League
Louis van Gaal            aliahidi kuipa taji Manchester United ndani ya miaka mitatu            lakini sasa ndoto hiyo inaonekana inaweza ikatimia katika            mwaka wake pili baada ya timu hiyo kuinyuka Sunderland 3-0.
        Katika mchezo huo            wa Premier League uliochezwa Jumamosi, United ilipata bao la            kwanza kupitia Memphis Depay kunako dakika ya 45 huku Wayne Rooney              akifunga bao lake la kwanza Ligi Kuu msimu huu katika dakika              ya 46 kabla ya Juan Mata kuifungia klabu hiyo bao la tatu              dakika ya 90 kwa shuti kali la karibu. 
        Rooney hakufunga bao lolote              Premier League tangu mwezi April msimu uliopita.
        Kwa ushindi huo Manchester United              imefanikiwa kuongoza msimamo wa Premier League kwa mara ya              kwanza tangu Sir Alex Ferguson alipostaafu kuikochi timu              hiyo mwaka 2013.
        Licha ya kutokufunga bao              katika mchezo huu, mshambuliaji mpya wa Manchester United Anthony              Martial ndiye aliyeng'ara zaidi.
          
                      
                    
          
        Manchester United (4-2-3-1): De              Gea 6.5; Valencia 5.5, Smalling 6, Blind 7 (Jones 74 6),              Darmian 6; Carrick 6.5 (Schweinsteiger 68 6.5), Schneiderlin              6; Mata 7, Rooney 6, Depay 6.5 (Young 77); Martial 7.5
          Sunderland (4-2-3-1): Pantilimon              6; Jones 6, O'Shea 6, Kaboul 5.5, van Aanholt 6; Cattermole              6, M'Vila 6; Johnson 5.5 (Fletcher 45 6), Toivonen 6              (Larsson 70 6), Lens 6.5; Borini 5.5
          Wayne Rooney akifurahi              bao lake la kwanza la Premier League tangu mwezi April
        Ni bao! Wayne Rooney              akiusindikiza kwa macho mpira uliotinga wavuni na kuwa bao              la pili kwa United
        
Comments
Post a Comment