Mwendo wa Manchester City katika Premier League unatisha - imeshinda mechi zake zote tano na kung'ang'ania kileleni mwa msimamo wa ligi.
Lakini pia City inaonekana ni yenye bahati baada ya kupata ushindi mwembamba dhidi ya Crystal Palace kupitia bao pekee la dakika ya 90.
Kinda wa miaka 18, Kelechi Iheanacho ndiye aliyekuwa lulu kwa Manchester City baada ya kufunga bao hilo pekee.
Crystal Palace (4-3-2-1): McCarthy 6.5; Kelly 6.5, Dann 7, Hangeland 6.5, Souare 7.5; McArthur 7.5, Puncheon 7 (Chung-yong 83, 6), Cabaye 7; Zaha 7, Sako 6.5 (Gayle 68, 6.5); Bolasie 7 (Jedinak 80)
Manchester City (4-2-3-1): Hart 7; Sagna 7, Kompany 8, Mangala 7, Kolarov 6.5; Fernandinho 6.5, Toure 7; Nasri 7 (Demichelis 90), Bony 6.5 (Iheanacho 89, 7), Navas 6.5; Agüero 6 (De Bruyne 25, 7)
Kelechi Iheanacho (katikati) akiifungia City bao pekee
Iheanacho akifurahia bao lake la muda wa lala salama
Kinda wa miaka 18 Iheanacho akiwa hoi kwa furaha
Comments
Post a Comment