LIVERPOOL ULIMI NJE KWA CARLISLE UNITED, YAPENYA KWA MATUTA …Southampton yaangusha karamu kwa MK Dons, pata matokeo ya mechi zote za Capital One
Kocha wa Liverpool aliye kikaangoni Brenden            Rodgers alilazimika kusubiri hadi hatua za matuta ili kusonga            mbele kwenye michuano ya Capital One dhidi ya timu dhaifu ya            Carlisle United.
        Liverpool walikuwa wa kwanza kufunga kupitia kwa            Danny Ings, lakini Carlisle United wakachomoa dakika 11 baadae            kwa bao la Derek Asamoah.
        Matokeo yakabaki hivyo hata pale ziliopoongezwa            dakika 30 za 'extra time' na ikabidi mshindi apatikane kwa            mikwaju ya penalti ambapo Liverpool ikashinda kwa 3-2.
        Nayo Southampton wamewaangushia kipigo kizito wababe wa            msimu uliopita wa Manchester United – MK Dons kwa kuwachapa            bao 6-0.
        Matokeo ya mechi zote za Capital One zilizochezwa            Jumatano ni kama ifuatavyo:
        Crystal Palace 4 - 1 Charlton Athletic
        Milton Keynes Dons 0 - 6 Southampton
        Newcastle United 0 - 1 Sheffield Wednesday
        Norwich City 3 - 0 West Bromwich Albion
        Tottenham Hotspur 1 - 2 Arsenal
        Walsall 1 - 4 Chelsea
        Liverpool  4            - 3 Carlisle United
        Manchester United 3 - 0 Ipswich Town
        
Comments
Post a Comment