KUFA KUFAANA ...MARCOS ROJO ANUFAIKA NA KUUMIA KWA LUKE SHAW



KUFA KUFAANA ...MARCOS ROJO ANUFAIKA NA KUUMIA KWA LUKE SHAW
Luke Shaw (centre)            suffers a double fracture of his right leg in a tackle by            Hector Moreno of PSV Eindhoven
Baada ya beki wa kushoto wa Manchester United, Luke Shaw, kuvunjika mguu wa kulia na kulazimika kuwa nje ya dimba kwa miezi sita, sasa Marcos Rojo njia nyeupe kurejea kwenye kikosi cha kwanza.

Shaw alipigwa daluga kali na Hector Moreno wa PSV Eindhoven ya Uholanzi katika pambano la kwanza Ligi ya Mabingwa Ulaya kwenye uwanja  Phillips jijini Eindhoven Jumanne usiku, ambako Mashetani Wekundu walilala kwa mabao 2-1, huku ikimpoteza beki huyo dakika ya 18.

Kocha wa Man United, Louis van Gaal, alifichua kuwa Shaw mwenye umri wa miaka 20, alikuwa akilia hadi vyumba vya matibabu na baadae vyumba vya kuvalia, pale alipoambiwa kwamba atakuwa nje ya uwanja kwa miezi sita.

Marcos Rojo beki wa kimataifa wa Argentina aliyekuwa na mgogoro na Van Gaal aliingia kuchukua nafasi ya Shaw.

Van Gaal amesema kuumia kwa Shaw ni pigo kubwa lakini akajipa moyo kuwa uwepo wa Rojo utasaidia kufunika pengo.

Kurejea kwa Rojo kunamaanisha kuwa Daley Blind atalazimika kwenda kucheza beki ya kushoto huku Rojo akiungana na Chris Smalling kuunda pacha ya beki ya kati.

"Mimi si daktari, ndio maana nakosa kauli rasmi ya lini atarudi uwanjani, lakini kimsingi unapovunjika mifupa miwili mikubwa, unakuwa na nafasi kubwa ya kupona baada ya miezi sita," alisema Van Gaal akionesha simanzi juu ya Luke Shaw.

Kabla ya Jumanne, Rojo hakuwa amecheza hata mchezo mmoja wa Manchester United msimu huu.




Comments