MSHAMBULIAJI na kipa mahiri wa zamani wa Yanga na Taifa            Stars, Kitwana Manara 'Popat' amesema kuwa umefika wakati kwa            Makocha wa Ligi Kuu kuwapa nafasi zaidi wachezaji wazawa            kuliko kuwabeba wageni.
        Manara aliseyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi            wa habari hizi jijini Dar es Salaam, ambapo alisema kuwa            amegundua baadhi ya wachezaji wakutoka nje ya nchi uwezo wao            mdogo.
        "Kweli wapo wachezaji wamesajiliwa kutoka nje ya nchi            uwezo wao ni mdogo, lakini wapo wachezaji wazawa wana uwezo            mkubwa ila hawapewi nafasi," alisema Manara.
        Amewaomba makocha hao kutoa nafasi zaidi kwa wachezaji            wazawa, ili waweze kuonyesha viwango kwenye michuano hiyo.
        Gwiji huyo amewasihi wachezaji wazawa nao kujituma ili            kuwafunika wageni kwani kinyume chake wataishia kucheza timu            za madaraja ya chini, kwa kuwa soka la sasa ni biashara hakuna            klabu itakayokubali kukaa na wachezaji mizigo. 
        "Hebu wachezaji wetu hapa nchini wabadilike na            wajitume, wasikubali kuozea benchi, wahakikishe wanapigania            namba kwenye vikosi vya kwanza," alisema.
        Alisema matatizo ya wachezaji kutojituma na kuozea            benchi, yanaighalimu nchi kwa timu ya taifa kutokuwa na            wachezaji wenye uwezo na wanaojiamini uwanjani, hivyo kufanya            vibaya kila kukicha.
        
Comments
Post a Comment