KIIZA AITUMIA SALAMU YANGA…



KIIZA AITUMIA SALAMU YANGA…
Hamisi Kiiza akishangilia goli la kwanza na wachezaji              wenzake wa Simba

Hamisi Kiiza (katikati) akishangilia goli la kwanza na wachezaji wenzake wa Simba kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Kagera Sugar mchezo ulipogwa kwenye uwanja wa Taifa

Hamis Kiiza 'Diego' ameendelea kufunga kwenye ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) baada ya leo kuifungia Simba magoli magoli yote matatu (hat-trick) kwenye ushindi wa goli 3-1 walioupata vijana wa Msimbazi kwenye uwanja wa Taifa wakati wakiwakabili Kagera Sugar kwenye mchezo wa raundi ya tatu ya ligi hiyo.

Goli la kwanza la Simba lilifungwa dakika ya 30 kipindi cha kwanza na Kiiza baada ya Awadh Juma kupiga pasi iliyomkuta Kiiza ambaye moja kwa moja aliukwamisha mpira wavuni.

Hamisi Kiiza (wapili kutoka kulia) akishanilia na              wachezaji wenzake mara baada ya kufunga goli la tatu

Hamisi Kiiza (wapili kutoka kulia) akishanilia na wachezaji wenzake mara baada ya kufunga goli la tatu

Goli hilo lilidumu kwa muda wote wa kipindi cha kwanza kwani hadi timu hizo zinakwenda mapumziko Simba walikuwa mbele kwa goli 1-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa Simba kufunga goli la pili mfungaji akiwa ni Hamisi Kiiza aliyefunga goli hilo dakika ya 46 kipindi cha pili.

Dakika ya 50 kipindi cha pili, Keneth Masumbuko aliifungia Kagera Sugar goli la pili baada ya mabeki wa Simba Hassan Isihaka na Justice Majabvi kutegeana kumkaba Masumbuko ambaye alifunga goli hilo kirahisi.

Kiungo wa Simba SC Peter Mwalyanzi (katikati) akijaribu              kuwatoka wachezaji wa Kagera Sugar

Kiungo wa Simba SC Peter Mwalyanzi (katikati) akijaribu kuwatoka wachezaji wa Kagera Sugar

Wakati muda ukiwa unaelekea kumalizika, Hamisi Kiiza alifunga goli la tatu katika dakika ya 90 na kuwa mchezaji wa kwanza kufunga hat-trick msimu huu.

Kwenye mchezo wa leo Simba walitengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini Ibrahim Ajib alipoteza nafasi nyingi za kufunga ambazo zingeweza kuwapa Simba magoli mengi mengi zaidi.

Ibrahim Job (mbele) akimiliki mpira mbele ya Hamisi              Kiiza 'Diego'

Ibrahim Job (mbele) akimiliki mpira mbele ya Hamisi Kiiza 'Diego'

Wachezaji wa Simba walioanza: Peter Manyika, Hassan Isihaka, Mohamed Hussen, Emery Nimuboma, Simon Serunkuma, Justice Mjabvi, Awadhi Juma, Said Hamisi Juma, Peter Mwalyanzi, Ibrahim Ajib na Hamis Kizza

Wachezaji wa akiba: Vicent Angban, Hassan Ramadhani, Said Issa, Mwinyi Kazimoto, Pape Abdoulaye Ndaw, Boniface Maganga na Joseph Kimwaga.

Peter Mwalyanzi wa Simba akiwania mpira na mcheaji wa              Kagera Sugar

Peter Mwalyanzi wa Simba akiwania mpira na mcheaji wa Kagera Sugar

Kikosi cha Kagera Sugar kilichoanza: Agathon Anton, Salum Kanoni, Said Hassan, Ibrahim Job, Deogratius Julius, George Kavilla, Iddy Kurachi, Laulence Mugia, Mbaraka Yussuph, Daudi Jumanne, Paul Ngaliyoma 8

Wachezaji wa akiba: Abuu Hashim, Aboubakari Mtilo, Erick Kihaluzi, Babuu Ally, Keneth Masumbuko, Lambele Jarome, Rashid Loshuwa.

Mashabiki wa Simba wakishangilia goli lililofungwa na              Hamisi Kiiza 'Diego'

Mashabiki wa Simba wakishangilia goli lililofungwa na Hamisi Kiiza 'Diego'



Comments