‘GOODBYE’ FLOYD MAYWEATHER


'GOODBYE' FLOYD MAYWEATHER
Mayweather alipiga magoti na kuangalia mbingu mara              baada ya kengele ya mwisho ya pambano lake dhidi ya Berto              kabla hajatangazwa kuwa bingwa

Mayweather alipiga magoti na kuangalia mbingu mara baada ya kengele ya mwisho ya pambano lake dhidi ya Berto kabla hajatangazwa kuwa bingwa

Bondia Floyd Mayweather alfajiri ya kuamkia leo alitazama mbingu kabla ya kutangazwa mshindi wa pambano lake analodai ni la mwisho katika career yake ya ngumi dhidi ya Andre Berto katika ukumbi wa MGM grand arena.

Akitoa ishara za kuaga kama alivyodai miezi kadhaa iliyopita, Floyd maarufu kama T.B.E 'The Best Ever' alitangazwa mshindi na majaji wote wanne, huku wawili wakimpa points 118/110 wengine, 117/111 na 120/108.

Ushindi wa Mayweather dhdi ya Berto umemfanya kuweka              rekodi ya kupigana mapambano 49 ila kupoteza

Ushindi wa Mayweather dhdi ya Berto umemfanya kuweka rekodi ya kupigana mapambano 49 ila kupoteza

Ushindi huo wa Floyd Mayweather unamfanya afikishe mapambano 49 bila kupigwa na kuweka historia ya aina yake huku ikizuka mijadala ya nani bondia bora wa muda wote katika ulimwengu wa ngumi.

Floyd Mayweather Jr amesema amefurahia jinsi 'carer'              yake ilivyokuwa na kamwe hawezi kurudi nyuma

Floyd Mayweather Jr amesema amefurahia jinsi 'carer' yake ilivyokuwa na kamwe hawezi kurudi nyuma

Katika pambano hilo, kama kawaida yake Floyd hakurusha makonde mengi kwa Berto na baada ya kurusha ngumi chache za ushindi akaanza kumkwepa mpinzani wake hadi pambano lilipofikia mwisho.

Mayweathe (kushoto) wakati akikabiliana na Berto              ulingoni

Mayweathe (kushoto) wakati akikabiliana na Berto ulingoni

Maswali yaliyopo hivi sasa ni je? Floyd kastaafu kweli? Hatorudi tena ulingoni? Tutasubiri kuona hilo kwa bondia ambaye ndiye mwenye pesa nyingi kuliko wanamichezo wote kwa ujumla wao.

Mayweather akifurahi na timun yake mara baada ya              kutangazwa mshindi dhidi ya Berto

Mayweather akifurahi na timun yake mara baada ya kutangazwa mshindi dhidi ya Berto



Comments