FARU JEURI WAFICHUA SIRI YA KUTWAA UBINGWA WA NDONDO CUP 2015


FARU JEURI WAFICHUA SIRI YA KUTWAA UBINGWA WA NDONDO CUP 2015
Gombela Athuman Katibu mkuu wa Faru Jeuri akielezea              jinsi walivyofikia mafanikio kwenye mchuano ya Ndondo Cup              msimu huu

Gombela Athuman Katibu mkuu wa Faru Jeuri akielezea jinsi walivyofikia mafanikio kwenye mchuano ya Ndondo Cup msimu huu

Naye katibu mkuu wa mabingwa wa michuano hiyo timu Faru Jeuri Bw. Gombela Athuman amesema, siri ya mafanikio yao hadi wanachukua ubingwa wa mashindano ya Ndondo Cup ni ushirikiano waliokuwa nao kwenye timu pamoja na kupanga mambo yao kwa pamoja.

"Ushirikiano ndio siri ya mafanikio yetu, tusingeweza kupata haya mafanikio kama tungekua hatushirikiani. Hakuna kitu kingine zaidi ya ushirikiano na kukaa kupanga mabo kwa pamoja", amesema Athuman.

Bi. Queen Mwaka (kulia) akimkabidhi katibu wa Faru              Jeuri Gombela Athuman (kushoto) kiasi cha shilingi milioni              tano wakiwa mabingwa wa Ndondo Cup 2015

Bi. Queen Mwaka (kulia) akimkabidhi katibu wa Faru Jeuri Gombela Athuman (kushoto) kiasi cha shilingi milioni tano wakiwa mabingwa wa Ndondo Cup 2015

"Zawadi hii tuliyoipata ya shilingi milioni tano tutatoa kiasi kidogo cha pesa kwa ajili ya kufanya sherehe ndogo ya kupongezana kwa wale wote tuliokuwa tunashirikiana sherehe ambayo inaweza ikafanyika siku ya Jumamosi na kiasi kitakachobaki tutakihifadhi benki kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao".



Comments