EVERTON YAWEKA REHANI KIBARUA CHA MOURINHO …bao 3-1 zamchanganya Roman Abramovich



EVERTON YAWEKA REHANI KIBARUA CHA MOURINHO …bao 3-1 zamchanganya Roman Abramovich
Naismith completed a perfect hat-trick - header,                right foot, left foot - to seal a memorable 3-1 victory                over the defending champions 
Hali si shwari Chelsea, kipigo cha ba0 3-1 kutoka kwa Everton kimechafua hali ya hewa huku ikionekana wazi jitihada za mabingwa hao kutetea taji lao, zinakumbana na vigingi vingi.

Tajiri asiye na subira Roman Abramovich, Ijumaa alikutana na kocha Jose Mourinho katika kile kilichobashiriwa kuwa ni gumzo kuhusu mwenendo wa timu, lakini matokeo haya ya Jumamosi yanatajwa kuwa yamezidi kumtia 'kizunguzungu' kibopa huyo wa Kirusi.

Steven Naismith aliyetokea benchi, akawa mwiba kwa Chelsea pale aliposimika mabao yote matatu ya Everton kwenye mchezo huo mkali wa Premier League.
Mashabiki wa Everton waliofurika kwenye uwanja wao wa Goodison Park, wakamdhihaki Mourinho kwa kumwimbia: "Unafukuzwa kazi kesho asubuhi", hiyo ikiwa ni baada ya Smith kufunga bao la tatu kunako dakika ya 83.

Smith aliyeingia dakika ya 9 kuchukua nafasi ya Muhamed Besic  nafasi ya aliyeumia, alifunga goli lake la kwanza dakika ya 17 kabla ya kutupia la pili dakika tano baadae huku kiungo Nemanja Matic akifunga bao pekee la Chelsea dakika ya 36.

Sentahafu kinda John Stones aliyewaniwa na Mourinho kwa udi na uvumba bila mafanikio, alikuwa kikwazo kikubwa kwa Chelsea.
All focus was on              Everton defender John Stones (centre) at the start of the              game after Chelsea failed to sign him this summer
 Sentahafu wa Everton John Stones (katikati) akiruka juu kuzuia mpira kwa kichwa

Hiki kinakuwa kipigo cha tatu kwa Chelsea tangu msimu huu uanze na kufanya ijikusanyie pointi 4 katika  jumla ya mechi tano na kuporomoka hadi nafasi ya 16 kwenye msimamo wa Ligi Kuu.

Everton (4-3-3): Howard 7, Coleman 7 (Funes), Jagielka 8.5 (c), Stones 8, Galloway 7, Barry 8, McCarthy 7, Besic 5 (Naismith 9), Barkley 7.5, Kone 7 (Lennon 6), Lukaku 7.5


Chelsea (4-2-3-1): Begovic 7; Ivanovic 4, Zouma 5, Terry 5 (c), Azpilicueta 5; Mikel 4 (Kenedy 5), Matic 8; Pedro 5 (Falcao 5), Fabregas 4 (Willian 5), Hazard 5.5; Costa 4
Substitute                    Naismith wheels away in celebration after handing                    Everton the lead in their Premier League clashNaismith akishangilia bao lake la kwanza
The Scotland                    forward doubled Everton's lead with a thunderous shot                    from outside of the area, as Branislav Ivanovic (left)                    stands off
 Naismith akitupia bao la pili kutoka nje ya 18
Naismith                    completed a perfect hat-trick - header, right foot,                    left foot - to seal a memorable 3-1 victory over the                    defending champions 
Hili goli la tatu la Naismith 
Chelsea                    midfielder Nemanja Matic pumps his fist after bringing                    the champions back into the game with a screaming                    long-range shot
Nemanja Matic akishangilia bao pekee la Chelsea




Comments