Brendan Rodgers            anapigania kibarua chake kufa na kupona baada ya wamiliki wa            Liverpool FSG kudaiwa kuanzisha mawindo ya kumnasa kocha wa            zamani wa Real Madrid Carlo            Ancelotti.
        Ancelotti, ambaye            alishinda taji la Mabingwa Ulaya akiwa na AC Milan na Real            Madrid,  amefuatwa ili kumbadili Rodgers ambaye amekuwa na            mwanzo mbaya msimu huu.
        Inaaminika            Rodgers bado anasapoti kutoka kwa baadhi ya watu wenye maamuzi            Liverpool, lakini sasa kibarua chake kipo kitanzini baada Ancelotti kutupiwa ndoano ili awe mrithi            wake.
        Liverpool inadaiwa              kusaka huduma ya kocha wa zamani wa  Real Madrid Carlo              Ancelotti baada ya Brendan Rodgers kuwa na mwanzo mbaya wa              msimu mpya
        Liverpool inajiandaa na              maisha bila Rodgers 
          
Comments
Post a Comment