BARCELONA BILA SUAREZ YAUA 4-1 ...MESSI APIGA 2, AKOSA PENALTI



BARCELONA BILA SUAREZ YAUA 4-1 ...MESSI APIGA 2, AKOSA PENALTI
Lionel Messi amefunga mara mbili na kukosa penalti moja wakati Barcelona ikiifumua Levante 4-1 katika mchezo wa upande mmoja wa La Liga.

Kwa ushindi huo Barcelona inazidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi 12 baada ya kushinda mechi zake zote nne.

Bao la kwanza la Barcelona lilifungwa na beki wake Marc Bartra katika dakika ya 50, Neymar akapiga la pili dakika 6 baadae kabla ya Messi hajafunga kwa penalti dakika ya 61 huku Levante wakifunga bao la pekee dakika ya 66 kupitia kwa Victor Casadesus.

Messi angeweza kufunga tena kwa penalti dakika ya 76 lakini shuti lake likapaa juu.

Dakika ya 90 uchu wa Messi ukazaa matunda pale alipoifungia Barcelona bao la nne.

Barcelona: Ter Stegen; Alves, Mascherano, Bartra, Adriano; Rakitic, Busquets, Sandro, Munir, Messi, Neymar.

Levante: Ruben, Ivan Lopez, Tono, Camarasa, Verza, Lerma, Juanfran, Roger, Trujillo, Ghilas, Feddal
Lionel Messi (left) and                  Neymar started for Barcelona without their third man in                  the 'MSN' trio - Luis Suarez - but they still won the                  game
Lionel Messi (kushoto) na Neymar wamecheza bila pacha wao Luis Suarez - lakini bado wakashinda
Marc Bartra was the unlikely                  provider of the first goal, slotting home nicely at the                  back post after a scooped pass from Messi
Marc Bartra akishangilia bao la kwanza
Messi (right) scored                  Barcelona's third goal in 11 minutes when he fired a                  penalty into the roof of the net in the second half
Messi (kulia) akiifungia Barcelona bao tatu kwa penalti
Following his goal, Neymar                  ran to the sidelines to collect a shirt with Rafinha on                  the back - the defender is out for the rest of the                  season
Neymar akimpa heshima beki wa Barcelona, Rafinha ambaye ni majeruhi na atakuwa nje ya dimba kwa msimu mzima


Comments