Alexis Sanchez            alirejea kwenye 'fomu' yake Jumamosi baada ya kuisaida Arsenal            kuinyuka Newcastle 5-2 huku akisukumiza wavuni mabao matatu            (hat-trick) kwenye mchezo safi wa Premier League. 
        Kwa alichokifanya            Sanchez Jumamosi, akaingia kwenye rekodi ya aina yake baada ya            kuwa mchezaji wa kwanza kupiga hat-trick kwenye ligi kuu za            Italia (Serie A), Hispania (La Liga) na England (Premier            League.
        Hat -trick ya            kwanza ya Sanchez  ilianzia Italia wakati akiichezea Udinese,            February 2011 ambapo alifunga mara tatu katika ushindi wa 7-0            dhidi ya Palermo.
        Miezi mitano            baadae kiwango chake kikaivutia Barcelona ya Hispania na            kumsajili kwa pauni milioni 23.
        January 2014            Sanchez akaipigia Barcelona hat-trick kwenye dimba la Nou Camp            katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Elche. 
         Alexis Sanchez amekuwa              mchezaji wa kwanza kupiga hat-trick Italia, Hispania na              England 
        Sanchez alianza kupiga              hat-trick Udinese ya Italia mwaka 2011 dhidi ya Palermo
        Sanchez akafunga              hat-trick yake ya pili Hispania akiwa na Barcelona  January              2014 dhidi ya Elche
          
Comments
Post a Comment