Miamba ya kandanda            Tanzania bara, Dar es salaam Young Africans imeendelea            kuinyanyasa Mbeya City FC baada ya jioni ya leo kuichapa 3-2            katika mechi ya kirafiki iliyochezwa uwanja wa Sokoine jijini            Mbeya.
        Magoli ya Yanga            yamefungwa na Mbrazil, Andrey Coutinho, Mrundi, Amissi Tambwe            na Mzimbabwe, Donald Ngoma, wakati magoli ya Mbeya City            yamefungwa na Bakari Mwinjuma na Meshack Samuel.
        Hiki ni kipigo cha tatu            cha aina hiyo kwani msimu uliopita katika mechi mbili za ligi            kuu, Yanga ilishinda 3-1 uwanja wa Taifa na ikapata ushindi            kama huo uwanja wa Sokoine.
        Msimu wa 2013/2014 ambao            Mbeya City waliishia nafasi ya tatu walitoka sare ya 1-1            uwanja wa Sokoine na wakafungwa 1-0 uwanja wa Taifa.
        Kwa lugha rahisi, Mbeya            City wanaendelea kuwa wateja wa Yanga iwe mechi za mashindano            au kirafiki.
        
Comments
Post a Comment