Wakati anacheza ligi kuu            ya England akiwa na timu za Chelsea na Everton, Samuel Eto'o            alionekana kuwa mshambuliaji hatari, ingawa makali yake            hayakuwa kama zamani.
        Pia Eto'o alionesha uwezo            mkubwa alipocheza  klabu ya Mallorca,
        Mwisho wa yote, kazi            kubwa aliyoifanya Barcelona, Cameroon na Inter Milan huiwezi            kusahaulika.
        Umri ukiwa umeenda (miaka            34), Mcameroon huyo ameenda Uturuki kumalizia soka lake.
        Jana usiku, alicheza            mechi ya kwanza katika klabu yake ya Antalyaspor na kufunga            magoli mawili katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Istanbul            Basaksehir.
        Katika dakika ya 50, Eto'o  aliufanya ubao usomeke              2-1 akifunga goli maridadi mno.
          Dakika 14 baadaye, alifunga goli lingine kwa ufundi              wa hali ya juu.
          Tazama video ya magoli ya Eto'o
        
Comments
Post a Comment