PICHA NA VIDEO: GOLI LA BENTEKE LAMKERA GARY NEVILLE




PICHA NA VIDEO: GOLI LA BENTEKE LAMKERA GARY NEVILLE
2B72760700000578-0-image-a-15_1439840527611
Gary Neville ameponda makosa endelevu ya kushindwa kutafsiri sheria mpya ya kuotea katika michuano ya ligi kuu England kufuatia Liverpool kupewa goli lisilostahili kwenye mchezo wa EPL uliopigwa Jana usiku dhidi ya Bournemouth.
Goli pekee la Christian Benteke katika uwanja wa Anfield lilitakiwa kukataliwa kwasababu mchezaji mwenzie, Philippe Coutinho alikuwa tayari ameotea.
Siku chache kabla ya msimu mpya kuanza, yalifanyika mabadiliko ya sheria ya kuotea ambapo mchezaji yoyote anayecheza mpira katika eneo la kuotea, kibendera lazima kiwe juu na hata kama hakugusa mpira.
Philippe Coutinho was clearly offside when the                    cross came in from the left wing from Jordan                    Henderson
Coutinho made an attempt to go for the cross                    before it reached Benteke at the far post but no flag                    was raised
Mwamuzi msaidizi,  Harry Lennard alishindwa kunyosha kibendera, akimuacha Benteke afunge.
Neville amedai makosa haya ni stori za kila msimu na kila msimu mpya wanakuja na mabadiliko lakini hakuna wanachofanya.



Comments