Na Salym Juma
Baada ya kuchoka na            mihangaiko ya kila siku niliamua kuchukua Kompyuta pakato            (laptop) na kuangalia video za soka ambazo zinatazamwa sana            mitandaoni. Mara nyingi napenda kuangalia zile ambao            hazizungumzwi lakini ni kali..! Nilijikuta naangalia video            moja kati ya Belgium na Bosnia..!
           Hapa Mtangazaji anatangaza goli 1 hadi analia kwa            furaha…! Goli hili ni la Mzungu mmoja aliyevaa jezi namba 11            anawalamba vyenga Mabeki kibao anafanya kama anapiga, kumbe            anapita.., anapiga mashuti makali sana, nawaona mabeki wa            Belgium wanachanganyikiwa mwisho anatupia goli kwenye nyavu            kule juu kabisa wanapotagia Ndege……
 Kutokana na kiwango cha huyu jamaa nalazimika            kumsikiliza 'Comententor' kwa makini ili kufahamu jina la huyu            Mzungu mrefu mwembamba ambaye nasikia imani yake ya dini ni            ile ya akina Franky
           Ribery na Adnan Januzaji..! Japokuwa 'Comentetor'            anatangaza hili goli kwa hisia ila mwisho nasikia jina lake…!!            duuu.! kumbe ni huyu……
Aliwahi kuwa Mchezaji wa kwanza kuifungia Man City magoli manne katika mechi moja kwenye EPL. Kwa mwaka 2011 usajili wake kuja EPL ndio usajili wa pili kwa ukubwa baada ya ule wa Robinho, pia ulikuwa usajili mkubwa kwa pale Bundesliga. Kipindi cha nyuma alikuwa anacheza nafasi ya kiungo..! Kuna katuni ya gazeti moja la Italia ilimuonesha akimpigia simu Tevez kuwa anakwenda Italia muda mchache baadae Tevez akaanza kutafuta dili la kurudi kwao…..
Hapa namzungumzia raia wa Bosnia aliyekuwa anawindwa na Jose Mourinho kwa muda mrefu, naomba tuwe wote hadi mwisho wa makala hii kuzungumzia 'point' hii ya Mourinho na Dzeko, nukta ambayo 'media'nyingi za Ulaya zimekaa kimya hadi leo licha ya kufahamu ni kwa jinsi gani Mou anamkubali Dzeko..
 "Mchezaji wangu bora wa mwaka siku zote anatokea            kwenye timu iliyochukua ubingwa. Ninasema mchezaji wa Man City            Dzeko. Alikuwa ni mshambuliaji chaguo la tatu mwanzoni mwa            msimu wakati timu inamuhitaji
           na alionesha tofauti. Alikuwa na magoli 16. Kumi na            sita kwa mshambuliaji chaguo la tatu ni jambo la kuvutia. Sio            mfungaji pekee pia anatoa assists na anacheza vizuri".
"Ana tabia nzuri, yupo fair, hajirushi ovyo uwanjani, hapendi kuwatafutia wapinzani kadi" Alimaliza Mourinho maneno haya siku ya Jumapili tarehe 10/5/2014.
 Akiwa Wolfsburg Eden alikuwa ni miongoni mwa            washambuliaji kuntu kwani katika mechi 32 za msimu wake wa            pili alitupia magoli 26 na kutoa assists 10. Kutokana na            kiwango hiki, timu yake ilichukua ubingwa wa
           ligi kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa timu hiyo.            Pia kama kumbukumbu zako ziko vizuri utakumbuka kipindi hiki            alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa Bundesliga hii ilikuwa baada            ya kutupia magoli sita katika mechi mbili za DFB-Pokal, magoli            manne na assist mbili katika mechi nane za UEFA.
 Pia hapa hapa Ujerumani alikuwa mfungaji bora wa ligi            na kukataa ofa ya kujiunga na klabu ya Ac Milan. msimu wake wa            mwisho akiwa Ujerumani alitupia magoli 10 katika mechi 17 huku            akitengeneza historia kwenye timu yake baada ya kutupia magoli            59 katika mechi 96..! Nani mwingine
           amefanya hivi pale Wolfsburg?? Hapa ndio Roberto            Mancini alipotokwa udenda na  kutoa pauni milioni 27 kumvuta            Etihad huku ukiwa usajili wa juu kufanywa na Man City kwa            kipindi hiki cha 2011 baada ya ule wa Robinho kutoka Madrid.            Hapa ndipo alipokuja kuanza safari yake kwa shida sana EPL            hadi alipoondoka sambamba na mwenzake Jovetic.
 Edez Dzeko alikutana na washambuliaji hatari duniani            "World class
           strikers" pale Etihad, kumbuka kipindi hiki walikuwepo            Baloteli (Super Mario),Tevez na Aguero..! Kwa viwango vya watu            hawa unadhani Eden angepata nafasi kama ile aliyokuwa anaipata            Wolsfburg? Hapa ndio mahali kiwango chake cha kutupia nyavu            kikaanza kushuka. Japokuwa alikuwa na wakati mgumu kumbuka            alikuwa mfungaji bora wa Man City msimu wa 2012-13 akiwa na            magoli 15 katika mechi 44. Hata baada ya kuondoka Tevez na            Baloteli bado washambuliaji wenye viwango kama Jovetic na            Wilfred Bony walikuja kuzidi kuhatarisha maisha yake pale            Etihad.
 Japokuwa mwaka jana alisaini mkataba mpya ni wazi kuwa            Dzeko amechoshwa na kusubiri mpaka Aguero, Jovetic na Bony            wasiwe vizuri ndipo apate uhakika wa kucheza muda wote,            kutokana na usajili wa
           Raheem ambaye inasadikika ataenda kuwa 'partner' wa            Aguero ni jambo la kheri Pellagrin kumruhusu aende akatafute            maisha mapya kwenye ligi ya Italia baada ya As Roma kumsajili            kwa pauini milioni 14, japokuwa alikuja kwa pauni milioni 27            sio mbaya kuondoka kwani kafanya kazi nzuri kwa kutupia magoli            72 katika mechi 187, kumbuka mechi nyingi alikuwa anatokea            kama 'sub' hapo ndo utajua uwezo wa huyu jamaa ambaye anatoka            Bosnia…!
 Tuachane na hayo ya Dzeko, sasa naomba tumuangalie            Jose Mourinho..! Tangu kurudi darajani bado hajapata 'striker'             wa uhakika hasa kutokana na Diego kuwa na 'Pancha' za mara            kwa mara. Louic Remy bado ni wale
           wale kama Diego.! Nilishangaa sana Mou kumuacha Dzeko            aende zake na kumchukua kwa mkopo Falcao. Japokuwa umri wa            miaka 29 ni ngumu Chelsea kukupa mkataba mnono ila ili kuweza            kupata magoli 20 ya uhakika kwa msimu ni wazi Jose alipaswa            kumshawishi kipenzi chake Dzeko kwenda darajani na kuwa chaguo            la pili baada ya Costa.
Japokuwa Aguero ni mshambuliaji hatari ila hadi kesho Mou anaamini Dzeko ni bora kama akipata nafasi muda wote. Kumbuka Chelsea mchezaji akiwa na miaka 30 hupewa mkataba wa mwaka mmoja, Dzeko ana miaka 29, hapa ndio palileta utata..! Pia kuna taarifa za chini chini kuwa City walikataa kumuuza Dzeko darajani kwa kuwa Chelsea ni wapinzani wao kwenye mbio za ubingwa licha ya Mou kumtaka Dzeko kimya kimya bila kuweka wazi hadharani, kumbuka kuna kipindi usajili wa Falcao kuja Chelsea ulitulia hadi watu wakasahau, kipindi hiki Mou ndo alikuwa ana 'fight' kumchukua Dzeko bila mafanikio..!
 Japokuwa Dzeko kaondoka na kushindwa kunaswa na Jose,            ni busara aende kuwafundisha adabu mabeki wa Serie A na            hatimaye kumaliza msimu akiwa na magoli zaidi ya 20, kuna            uwezekano Dzeko akaenda kufanya makubwakwani pale Roma atakuwa            na uhakika wa kucheza kwa uhuru japokuwa mshahara wake utakuwa            mdogo tofauti na ule wa pale Etihad. Kila lakheri 'brother'            Dzeko Mungu akutangulie sisi mashabiki tunasubiri
           makubwa kutoka kwao maana kipaji chako hakielezeki.
Comments
Post a Comment