JEZI MPYA YA MANCHESTER UNITED IMEVUJA REKODI YA MAUZO YA MEGASTORE



JEZI MPYA YA MANCHESTER UNITED IMEVUJA REKODI YA MAUZO YA MEGASTORE

2B02400900000578-3033827-image-m-10_1438610075294

Megastore ndipo jezi original mpya za Manchester united by Adidas zilipoanza kuuzwa. Manchester united ndio wanashikilia rekodi ya kuwa na mkataba wa gharama kubwa zaidi wa kutengeneza jezi ambapo mkataba wao una thamani ya £750m kwa muda wa miaka 10.

Mmoja kati ya maboss wa Adidas Herbert Hainer ametoa taarifa kwa njia ya conference call kwamba jezi hizo mpya za Adidas zimevunja rekodi ya 50% kutoka kwenye rekodi iliyokuwepo mwanzo.

Boss huyo amesema jezi hizo zimeuzika sana ikiwa hata mechi hazijaanza. Wakati mechi zikianza demand ya jezi itaongezeka kwa mashabiki watakao hitaji kwa ajili ya kwenda uwanjani wamevaa. Hivyo basi kuna tegemeo kubwa la kuongezeka kwa mauzo ya jezi hizo.



Comments