CHRISTIAN BENTEKE AANZA KWA MAKEKE LIVERPOOL, APIGA BAO KATIKA MECHI YAKE YA KWANZA



CHRISTIAN BENTEKE AANZA KWA MAKEKE LIVERPOOL, APIGA BAO KATIKA MECHI YAKE YA KWANZA
Christian Benteke aliyesajiliwa Liverpool kwa pauni milioni 32.5, ameanza vema kuitumikia timu yake mpya baada ya kufunga bao tamu kwenye mchezo wake wa kwanza kwenye kikosi cha Brenden Rodgers.

Liverpool imeeshinda 2-1 Swindon katika mchezo wake wa mwisho wa maandalizi ya msimu mpya, ambapo Benteke aliyesajiliwa kutoka Aston Villa alifunga bao la kuongoza dakika ya 48.

Jonathan Obika akaisawazishia Swindon dakika 27 kabla ya mchezo kumalizika, lakini Sheyi Ojo akaifungia Liverpool bao la ushindi katika dakika ya 87.

Belgium international                  Christian Benteke leaps in the air after scoring 48                  minutes into his Liverpool debut 
 Christian Benteke akishangilia bao lake
Roberto Firmino celebrates                  with his new team-mate following the Liverpool striker's                  opening goal
Roberto Firmino akimpongeza Benteke
Benteke's volley flew past                  Swindon goalkeeper Lawrence Vigouroux, who could only                  stand and stare
Benteke akifunga kwa shuti kali







Comments