Arsenal wakiwa            kwenye uwanja wao wa nyumbani, wamelazimishwa sare ya 0-0 na            Liverpool katika mchezo mgumu wa Premier League.
        Liverpool            walitawala vizuri katika dakika 45 za kwanza lakini kipa wa            Arsenal Petr Cech              aliyeng'ara vilivyo akawa shujaa kwa kuondoa michomo ya              hatari kutoka kwa Christian Benteke na              Philippe Coutinho.
        Hata hivyo ni Arsenal              watakaoumizwa zaidi na sare hii baada ya kiungo Aaron Ramsey kufunga bao              safi dakika ya 9 lakini kwa mshangao wa wengi mwamuzi Michael            Oliver akalikataa kwa madai ya kuwa mfungaji alikuwa ameotea.
        Liverpool bado            hajaifungwa hata goli moja tangu msimu huu ulipoanza baada ya            kushinda  mechi zake mbili za mwanzo dhidi ya Stoke City na Bournemouth.               
        ARSENAL (4-2-3-1): Cech;            Bellerin, Chambers, Gabriel, Monreal; Coquelin            (Oxlade-Chamberlain 82mins), Ramsey; Ozil, Cazorla, Sanchez;            Giroud (Walcott 73)
        LIVERPOOL (4-3-3): Mignolet;            Clyne, Lovren, Skrtel, Gomez; Can, Milner, Lucas (Rossiter            76); Coutinho (Moreno 88), Firmino (Ibe 63), Benteke.
        Petr Cech akiruka na kupangua kwa mkono wa            kushoto shuti la karibu la  Benteke
        
Comments
Post a Comment