RAHEEM STERLING AANZA KUKUNJUA MAKUCHA LIVERPOOL, AJIPANGA KULAZIMISHA UHAMISHO


RAHEEM STERLING AANZA KUKUNJUA MAKUCHA LIVERPOOL, AJIPANGA KULAZIMISHA UHAMISHO
Raheem Sterling amekunjua makucha yake na kuwaambia Liverpool kuwa hataki kuandamana na timu hiyo katika ziara yao ya mashariki ya mbali.

Licha ya winga huyo kushiriki mazoezi ya kujindaa na msimu mpya, lakini anataka kubaki England ili ajipange na mpango wake wa kutaka kuihama Liverpool.

Raheem ameonyesha wazi kuwa hana nia ya kuendelea kuitumikia Liverpool na sasa anaingia kwenye hatua ambayo inaonekana kama ni mwelekeo wa kulazimisha kuuzwa.

Manchester City bado haijapeleka ofa ya tatu huku mbili zikiwa zimepigwa chini na Liverpool ambayo inataka ilipwe pauni milioni 50 kwa kinda huyo wa miaka 20.

Andre Wisdom and Raheem                  Sterling (front) in pre-season training with Liverpool                  on Monday 
Andre Wisdom na Raheem Sterling (mbele) wakiwa mazoezini siku ya Jumatatu
Sterling reported to Melwood                  Training Ground on July 6 despite is intention to leave                  Anfield
Sterling ameripoti Melwood Training Ground  Julai 6 licha ya mipango yake ya kutaka kutimka Liverpool
Sterling arrived at                    training in a white Mercedes to begin pre-season                    training before the 2015-16 campaign
Sterling akiwasili mazoezini na Mercedes yake nyeupe
Liverpool rejected an                    improved offer for Sterling, from City, of £35million                    rising to £40million last month
Liverpool imeshakataa ofa mbili za Manchester City £35million na  £40million 


Comments