Mesut Ozil            amekabidhiwa jukumu la kucheza kama namba 10 likiwa ni jukumu            lake jipya kwa msimu ujao.
        Hiyo ni hatua ya            kocha wa Arsenal Arsene Wenger ya kutafuta njia sahihi ya            kumfanya mchezaji huyo aliyenunuliwa kwa pauni milioni 24            aonyeshe uwezo wake uliotarajiwa na wengi.
        Ozil anayeshikilia            rekodi ya usajili wa bei mbaya kwa Arsenal alikuwa            akichezeshwa katika mfumo wa viungo washambuliaji watatu ambao            ulishindwa kumweka katika ubora wake.
        Lakini sasa            atacheza nyuma ya mshambuliaji namba 9 huku Alexis Sanchez akihamishiwa              kucheza kama winga.
        Mesut Ozil (katikati)              sasa atacheza kama namba 10
        Ozil ameshindwa              kung'ara Emirates katika nafasi ya kiungo
        
Comments
Post a Comment