MARCOS ROJO anaamini Angel Di Maria ndiye              mchezaji mwenye kipaji zaidi katika Manchester United na              anaamini winga huyo atarejea kwenye uhalisia wake msimu              ujao.
          Di                Maria alijunga na Manchester United kiangazi kilichopita                akitokea Real Madrid kwa pauni milioni 59.7 ambayo ilikuwa                rekodi mpya ya usajili Uingereza, lakini kinyume na                matarajio ya wengi, akashindwa kung'ara Old Trafford.
          Nyota                huyo mwenye umri wa miaka 27 alifunga magoli matatu katika                mechi zake tano za mwanzo lakini hali ikageuka baadae na                akakumbwa na ukame wa magoli huku akiandamwa na majeraha                ya mara kwa mara.
          Lakini                mchezaji - Marcos Rojo - anayekipiga na Di Maria katika                timu ya taifa ya Argentina na Manchester United, anasema                anaamini makali ya mshambuliaji huyo yatarejea sehemu yake                msimu ujao.
        
Comments
Post a Comment