MARCOS ROJO ASEMA MCHEZAJI MWENYE KIPAJI ZAIDI MANCHESTER UNITED NI ANGEL DI MARIA


MARCOS ROJO ASEMA MCHEZAJI MWENYE KIPAJI ZAIDI MANCHESTER UNITED NI ANGEL DI MARIA
MARCOS ROJO anaamini Angel Di Maria ndiye mchezaji mwenye kipaji zaidi katika Manchester United na anaamini winga huyo atarejea kwenye uhalisia wake msimu ujao.
Di Maria alijunga na Manchester United kiangazi kilichopita akitokea Real Madrid kwa pauni milioni 59.7 ambayo ilikuwa rekodi mpya ya usajili Uingereza, lakini kinyume na matarajio ya wengi, akashindwa kung'ara Old Trafford.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 alifunga magoli matatu katika mechi zake tano za mwanzo lakini hali ikageuka baadae na akakumbwa na ukame wa magoli huku akiandamwa na majeraha ya mara kwa mara.
Lakini mchezaji - Marcos Rojo - anayekipiga na Di Maria katika timu ya taifa ya Argentina na Manchester United, anasema anaamini makali ya mshambuliaji huyo yatarejea sehemu yake msimu ujao.
Marcos              Rojo has backed Angel Di Maria to show his best form next              season
SAPOTI: Marcos Rojo anaamini Angel Di Maria atarejea kwenye ubora wake msimu ujao
"Kwangu mimi, mchezaji mwenye kipaji zaidi Manchester United ni Angel"
Marcos Rojo
"Kwangu mimi, mchezaji mwenye kipaji zaidi Manchester United ni Angel," Rojo aliliambia Goal.
"Kuna wachezaji wengi wazuri ndani ya United, lakini kwangu Di Maria ni mmoja wa wachezaji bora klabuni na ulimwenguni.
"Ulikukwa mwaka mbaya kwake. Alipata shida kuzoea mfumo wa timu lakini hilo ni jambo la kawaida.
"Mchezaji yeyote anayeingia kwenye nchi mpya na ligi mpya anapaswa kukabiliana na tofauti zinazojitokeza, hilo huwa linatokea. Naamini atakuwa ameimarika msimu ujao."


Comments