MANUEL PELLEGRINI AWEKWA KIKAANGONI MANCHESTER CITY ...Pep Guardiola apiga endiketa



MANUEL PELLEGRINI AWEKWA KIKAANGONI MANCHESTER CITY ...Pep Guardiola apiga endiketa
MANUEL PELLEGRINI anaingia kwenye mgongano mkubwa na mabosi wa Manchester City juu ya hatma yake ndani ya Etihad.


Pellegrini is fighting for his                City future
MSUGUANO: Pellegrini anapigania hatma yake Etihad 
Kocha huyo raia wa Chile aliponea chupuchu kutimuliwa kiangazi hiki licha ya kumaliza bila taji lolote.
Lakini inaeleweka kuwa mwenyekiti wa Manchester City Khaldoon Al-Mubarak amepania kumchukua kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola miezi 12 ijayo.
Kwa hali hiyo, Pellegrini anaweza akajikuta anaitumikia City kwa mwaka wa mwisho kwa vile klabu hiyo haijaonyesha dhamira ya kurefusha mkataba wake. 
City are keen on bringing                  Guardiola to the Etihad
ANATAKIWA: City inamsubiria Guardiola kwa miezi 12 ijayo
Khaldoon Al-Mubarak amepania kufanya usajili wa kishindo kiangazi hiki, hali inayompa imani Pellegrini kuwa anaweza kuwa na kikosi kizuri kitakachookoa kibarua chake.
Pellegrini, 61, anaamini anaweza akashinda taji la Premier League pamoja na Champions League na hivyo kuwa kishawishi cha kupewa mkataba mpya.
Khaldoon Al-Mubarak amepania kumchukua kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola miezi 12 ijayo



Comments